Saturday 25th, June 2022
@Uwanja wa Uhuru
Tanzania husherehekea maadhimisho ya Uhuru tarehe 9 Desemba kila mwaka. Katika siku hii mwaka 1961, Tanzania wakati huo Tanganyika ilipata uhuru kutoka kwa Uingereza.
Siku hiyo, Desemba 9, kulikuwa na fashifashi, shamrashamra na furaha jijini Dar es Salaam. Sherehe rasmi zilifanyika Uwanja wa Taifa na wakati huo huo kulikuwa na Mwenge wa Uhuru uliopelekwa kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro.
Kwa heshima ya mafanikio haya ya kihistoria, Serikali inafuatilia sekta zake kwa kutaja mafanikio yake, matatizo na changamoto ilizozikabili tangu Uhuru na kupanga mwelekeo wa baadaye. Mwaka 2021 Tanzania inaadhimisha miaka 60 ya Uhuru kwa kauli mbiu ya: "Tanzania imara, Kazi iendelee."
Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania
Telephone: +255232110038
Simu ya Mkononi: +255784494689
Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz
Copyright ©2021 MkurangaDc. All rights reserved.