• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Tasks MIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Idara ya fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi Au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mifugo na Uvuvi

Kutafsiri na kusimamia sheria, kanuni, sera, miongozo na taratibu mbalimbali za sekta za mifugo na uvuvi kitaifa ili kuhakikisha uwepo wa uzalishaji endelevu wa mifugo na mazao yatokanayo na mifugo na uvuvi katika wilaya kwa madhumuni ya kufikia malengo ya uzaalishaji kitaifa; Kushirikiana na wadau/washirika wa maendeleo (kama vile Taasisi binafsi na za umma) katika kutoa huduma shirikishi za ugani, kuanzisha na kuendeleza miradi ya uendelezaji mifugo na uvuvi katika wilaya; Kushirikiana na uongozi katika ngazi mbalimbali za kitaifa, Mkoa, Halmashauri na Idara nyingine katika kutimiza majukumu ya kila siku; Kushirikiana na wadau mbalimbali kudhibiti uingiza wa mifugo kiholela na kuzuia uvuvi haramu katika wilaya, kwa kufanya doria, kutoa leseni za uvuvi na kutoa elimu juu ya matumizi bora ya zana za uvuvi.

Kushauri na kuzisimamia serikali za vijiji kutenga maeneo ya malisho ili kuzuia migogoro inayoweza kutokea baina ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi katika vijiji; Kuwa daraja kati ya wafugaji na watafiti wa mifugo na uvuvi, kwa kuzitambua na kuchukua changamoto za wafugaji na kuzipeleka kwa watafiti ambao watazitafutia majibu muafaka na kurudisha/ kupeleka mrejesho kwa walengwa. Pia kusambaza teknolojia sahihi za kitaalam kutoka kwa watafiti kwenda kwa wafugaji ili kuongeza tija katika uzalishaji wa mifugo, samaki na bidhaa zake; Kudhibiti magonjwa mbalimbali ya mifugo, ikiwemo yale ya mlipuko na yale yanayo waathili binadamu kutoka kwenye mifugo, kama vile Kifua Kikuu, Kimeta, Kichaa cha Mbwa n.k, kwa kutoa tiba, chanjo, ukaguzi wa nyama na kutoa vibali vya kusafirisha mifugo. Pia kutoa taarifa za magonjwa ya milipuko, kuchukua na kupeleka sampuli za wanyama katika  kituo cha uchunguzi wa mifugo Temeke Dar es salaam; Kuhakikisha wataalam wa mifugo na uvuvi wenye sifa zinazo stahili wapo wa kutosha katika ngazi zote na wanahamasa ya kufanya kazi;

Kudhibiti ubora wa bidhaa za mifugo na uvuvi, pia kuhamasisha uongezaji thamani wa mazao ya mifugo na uvuvi na kusisitiza ufugaji wa kibiashara;  Kutafsiri na kuunganisha majukumu, matakwa na malengo ya wadau watoa huduma za ugani katika sekta za mifugo na uvuvi; Kutambua aina ya wafugaji na mahitaji yao muhimu katika maeneo mbalimbali; Kuendeleza matumizi ya mbinu za asili za ufugaji; Kuendeleza na kuboresha kosaafu za mifugo ya asili kwa uhamilishaji na kutumia madume bora ili kuongeza uzalishaji wa mifugo; Kukuza na kuimarisha mitandao miongoni mwa wadau wa kutoa huma za ugani na wafugaji wenyewe; Kukuza ushiriki wa wadau binafsi wa kutoa huduma za ugani, kutunza kumbukumbu na kufuatilia shughuli zao;  Kwa kushikiana na wadau wa maendeleo Kuwezesha ujenzi wa miundombinu ya mifugo na uvuvi katika maeneo ya wafugaji; Kukusanya, kuchambua, kutunza, kuboresha na kuzitumia taarifa/takwimu za mifugo na uvuvi katika kupanga mipango ya maendeleo na bajeti ya sekta katika wilaya; Kuhusisha na kushughulikia maswala mtambuka kama vile  jinsia, mazingira na VVU/UKIMWI.

MAFANIKIO YA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

  • Idadi ya Mifugo imeongezeka kwa 5.7%, 
  • Kulikuwa na mifugo 393,865 kabla ya Desemba 2015 hadi sasa kuna idadi ya  mifugo 417,671 kwa 2017
  • Udhibiti wa Magonjwa ya Mifugo 
  • Chanjo ya Mifugo
  • Idadi ya mifugo iliyochanjwa dhidi ya magonjwa mbalimbali ni 408,349  ambapo kati yao; Kuku 82,615, waliochanjwa dhidi ya Ndui, Kuku 323,117 walichanjwa dhidi Mdondo, Mbwa 2,451 na Paka 166  walichanjwa dhidi ya Kichaa cha Mbwa. Vile vile Ng’ombe 87 walikingwa dhidi ya Ndigana kali . Hii ni zaidi ya 9.97% ya ongezeko la mifugo iliyochanjwa ambapo kabla ya Desemba 2015 ni mifugo 371,326 tu ilichanjwa
  • Elimu kwa wafugaji imetolewa 
  • Wafugaji 147 wamepewa elimu juu ya ufugaji bora wa kuku wa asili
  • Wafugaji132 walipewa elimu ya ufugaji bora wa  mbuzi wa asili na
  • Wafugaji 15 walipewa elimu ya ufugaji bora wa  mbuzi wa  maziwa.
  • Hali ya mnada wa awali wa Mkiu imeimarika 
  • Wafugaji wamehamasika kupunguza mifugo kwa kuuza kwa faida kibiashara.hii inadhihirishwa na ongezeko la mifugo katika mnada wa awali wa Mkiu ambapo ni Mifugo chini ya 40 kwa siku ilikuwa ikiletwa mnadani kabla ya Desemba 2015 hadi sasa ni mifugo zaidi ya 120 inaletwa kwa siku.
  • Utambuzi, usajili na ufuatiliaji wa mifugo
  • Ng’ombe 11,467 wametambuliwa na kusajiliwa katika vijiji mbalimbali vya wilaya ya Mkuranga
  • Kushughulikia migogoro ya Wafugaji na Wakulima 
  • Kulikuwa na Migogoro ya wakulima na wafugaji abayo iliongezeka maradufu kutokana na uvamizi wa mifugo katika maeneo yasiyo ya ufugaji. Makundi yote ya wafugaji wavamizi yaliondolewa katika maeneo yaliyovamiwa na mifugo. Wakulima pia na wafugaji walielimishwa mahusiano mema kwa kuabiwa kila mtu aheshimu mipaka yake Wakulima wasiende kufanya shughuli za kilimo kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya Malisho na Wafugaji wasilishe mifugo yao kwenye maeneo yasiyotengwa kwa malisho.

Kutenga maeneo ya malisho 

  • Wilaya ya Mkuranga imetenga maeneo kwa ajili ya ufugaji Hekta 7,768.53 katika vijiji kumi (10) ambavyo ni Nyamato, Mkiu, Kilamba, Mbulani, Vianzi, Kizapala, Lupondo, Kibesa, Kisegese na Tundu.      
  • KUDHIBITI UINGIZAJI WA MIFUGO
  • Zoezi la kuwaondoa wafugaji wavamizi lilifanyika mara tatu, awamu ya kwanza mwezi Desemba 2016 ambapo jumla ya Ng’ombe 3,560 na Punda 3 waliondolewa, awamu ya pili mwezi Machi 2017 ambapo Ng’ombe 4,110, Mbuzi 60 na Punda 12 waliondolewa na awamu ya tatu ilifanyika mwezi Agosti 2017 ambapo jumla ya Ng’ombe 2,420, Mbuzi 57, Kondoo 35, na Punda 11 waliondolewa na kurudishwa walikotoka. Aidha katika zoezi la mwezi Agosti 2017 Ng’ombe 17 na  wafugji wavamizi 3 walikamatwa karika Misitu ya hifadhi ya Masanganya, Mkerezange na Kibesa. Wafugaji hao wamepelekwa mahakamani na mashauri yanaendelea.
  • VIKUNDI VYA WAFUGAJI
  • Wananchi katika kata zote wamehamasishwa kuunda vikundi vya ufugaji wa kuku na samaki hatimaye jumla ya vikundi 19 vya ufugji wa kuku vimeunda na kusajiriwa. Zoezi ni endelevu na wanchi wengine wako katika hatua mbalimbali za kuunda vikundi.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                       

CHANGAMOTO

Wananchi kushindwa kumudu gharama za madawa, chanjo, viuadudu kutokana na vitu hivyo kuuzwa kwa bei kubwa na hakuna ruzuku inayotolewa na serikali, vilevile dawa au chanjo zinapatikana maeneo ya mbali hivyo kuongeza gharama za usafiri.

Upungufu wa miundombinu ya mifugo kama vile Majosho ya mifugo, Malambo na Vituo vya Huduma za Afya za Mifugo.

Uwepo wa mimea yenye Sumu

Ufinyu wa bajeti

Wafugaji wavamizi kutoka nnje ya Wilaya ya Mkuranga.

  • UVUVI
  • MAFANIKIO
  •  Kupunguza Uvuvi haramu na hasa kwa wavuvi wanaotumia mabomu toka zaidi milipuko 1080 kwa mwaka kabla ya Desemba 2015 hadi chini ya milipuko 208 kwa mwaka kwa kipindi cha 2015 -2017
  •  Wavuvi wengi wamehamasika kukata leseni za uvuvi, wavuvi 323 wamekata leseni za uvuvi kwa mwaka 2016 - 2017 tofauti na 211 kwa 2014 -2015
  • Elimu ya ufugaji wa samaki imewavutia watu wengi kufanya ufugaji wa samaki. Zaidi ya wananchi 248 wamepewa elimu  ya ufugaji wa samaki katika mwaka 2016 – 2017 ikilinganishwa na 70 kwea mwaka 2014 – 2015. Hivyo kwa hiv sasa kuna mabwawa ya samaki wa maji baridi 93 kutoka 21 yaliyokuwepo kabla ya 2015.
  • Kupungua kwa hali ya utoroshaji wa rasilimali za Uvuvi na hasa usafirishaji haramu wa samaki hai na viumbe mbalimbali wa baharini
  •  Elimu juu ya zana bora za uvuvi imetolewa kwa wavuvi 33 katika Kata ya Kisiju, Magawa, na Shungubweni na elimu juu ya ufugaji bora wa samaki ilitolewa kwa wafugaji ishirini na sita (26) katika Kata za Vikindu, Mwarusembe, Mbezi na Mkuranga.
  • CHANGAMOTO
  • Bado kuna upungufu wa watumishi katika sekta ya Uvuvi kwa ngazi za Kata na Vijiji, tuna Maafisa Uvuvi watatu (3) tu mpaka sasa ambao hawatoshi kuhudumu katika vijiji 125



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA UALIMU YA MUDA MFUPI March 23, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA LA III March 21, 2023
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA AJIRA MPYA July 03, 2021
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA UDEREVA April 14, 2022
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • DED akutana na viongozi sekta ya Elimu Mkuranga

    January 15, 2023
  • Madiwani Mkuranga Wapitisha Bajeti ya TARURA

    December 22, 2022
  • Mkurugenzi Mkuranga akabidhi Madarasa kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga

    December 20, 2022
  • DED Mkuranga afanya ziara kukagua madarasa mapya ya sekondari

    December 19, 2022
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.