• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Sanga apongeza Juhudi za ANSAF

Posted on: August 28th, 2018

Mkuu wa wilaya ya mkuranga Mh. Filberto Sanga amepongeza jitihada zinazofanywa na jukwaa la wadau wakilimo (ANSAF) katika kuboresha afya na kipato cha wakazi wa wilaya hiyo

Sanga alisema hayo jana  wakati wakufunga rasmi awamu ya nne ya Mradi wa kusambaza mbegu bora za viazi lishe ‘Sambaza Mbegu Fasta’ (Fast Trade Project) ulio chini ya wizara ya kilimo Tanzania na Zanzibar na ufadhili wa mfuko wa Bill & Melinda Gates wa nchini Marekani.

Amesema anafurahishwa na nguvu iliyowekwa na shirika hilo katika kutoa elimu ya lishe kwa wananchi, kusambaza mbegu na kusimamia vyema shughuli za kilimo na pia utengenezwaji wa bidhaa mbalimbali zinazotokana na zao la viazi lishe.

Sanga pia aliwapongeza wananchi waliotumia fursa hiyo kujitengenezea kipato baada ya kusambaza mbegu za viazi nakuuza mazao ya viazi na bidhaa mbalimabali zitokanazo na zao hilo kama vile, unga wa lishe, tambi, keki, chapati, ‘juice’ ya viza lish na kadhalika pamoja na kuimarisha afya za familia zao.

Sanga alisema, anapendendekeza lishe hiyo ianze kutolewa katika shule za sekondari pia ilikuboresha afya za wanafunzi hao itakayopelekea kuboreka matokeo kitaaluma kwani wanafunzi wakiwa na uhakika wakupata chakula shuleni, itaboresha mahudhurio yao lakini pia Vitamin A inayopatikana kwa wingi katika zao hilo ni muhimu katika kuimarisha afya na akili pia.

Aliongeza kuwa imefika wakati kwa wanainchi hao kuunga mkono jitihada hizo kwa vitendo ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa watu wengine bila kusubiri vikao vya wataalamu hao kutoka ANSAF bali wale waliopata elimu hiyo awali watumike kuisambaza kwa watu wengine ili kuleta matokeo bora zaidi.

Naye Mkurugenzi wa kituo cha utafiti wa miwa – Kibaha (Sugarcane Research Institute - Kibaha) Dr. Kiddo Mtunda akielezea mafanikio ya mradi huo unaoshirikiana na vituo vya utafiti wa kilimo Mikocheni, Kizimbani na KOLPING, alisema viazi lishe ni zao muhimu kwaTanzania na linashika nafasi ya pili likitanguliwa na zao la mihogo katika mazao ya mizizi. Na kama likilimwa vema linaweza kutokomeza kabisa tatizo la uhaba wa chakula na lishe bora katika familia.

Dr. Kiddo alisema katika mradi huo wa ‘Sambaza mbegu fasta’ kinachofanyika ni kugawa mbegu katika wilaya hiyo kwa kutumia wanafunzi wa shule za msingi kwa kuchagua wanafunzi 200 wanaotoka kaya tofauti, “Tunawapa mbegu 120 kila mmoja zikiwa kwenye makundi manne tofauti, kisha kuwaagiza wanafunzi hao kuwapa wazazi wao ambao nao hupata mafunzo ya kuzipanda”

Alisema kwa asili wakulima walizoea kulima viazi vitamu vyenye rangi nyeupe au ya maziwa kwa ndani lakini kuna viazi vyenye rangi ya karoti kwa ndania mbavyo vina vitamini A kwa wingi. Kutokana na kuwa na vitamiani A kwa wingi ni faida kwa afya ya macho, ngozi, ukuaji bora na pia huimarisha kinga ya miili yetu dhidi ya maradhi, “vitamin A zenye karotini husaidia sana kusafisha mwili na kutukinga dhidi ya maradhi na kuzeeka kabla ya wakati wetu”,

mbali na utaratibu wa kuhamasisha uzalishaji wa mbegu bora na safi za viazi lishe kwa kuwatumia wanafunzi wa shule za msingi kufikisha mbegu hizo katika familia zao, lakini pia kutakua na uelimishaji wa wanafunzi hao kupitia vibonzo/katuni ziyakazoandaliwa na msanii Masoud Kipanya kwa kuaandaa vitabu vitakavyosambazwa shuleni.

Akizungumzia ufanisi wa mradi huo huku akimtolea mfano mkulima Festus Sebastian Dr. Kiddo anasema zao hilo likizalishwa kwa njia bora sio tu husaidia kupata chakula cha uhakiaka bali ni fursa nzuri kibiashara kwa ziada inayobaki kwani gunia moja la viazi lishe linauzwa kwa Tsh30000 hadi Tsh40000.

Lengo hili litasaidia kupunguza kama si kumaliza kabisa matatizo ya uhaba wa chakula na kushambuliwa na maradhi.

Naye mtaalamu wa lishe kutoka chuo cha utafiti wa kilimo Mikocheni (MARI) Bi. Domina Nkuba, alielezea umuhimu wa lishe hiyo kwa watoto, wanawake wajawazito na wanaonyonyesha pamoja na wanaume na kutoa takwimu za mafanikio “mpaka sasa tumeshatoa elimu kwa wakulima 624 kati yao wanawake ni 277 ndani ya wilaya ya mkuranga lakini elimu hiyo pia ilitolewa kwa maafisa Afya, walimu na maafisa lishe”

Wakati huohuo alikabidhi nakala za vitabu 1200 kwa mgeni rasmi wa mkuu wa wilaya kwaajili ya kuvisambaza katika shule za ndani ya wilaya hiyo ikiwa ni mpango wakueneza elimu zaidi juu ya faida ya zao la viazi lishe na pia kuwaelimisha wananchi juu ya mgawanyiko sahihi wa makundi ya vyakula kwani kumekua na uelewa tofauti katika jamii juu ya makundi hayo.

Alisema uelewa juu ya elimu ya lishe na matumizi sahihi umeendelea kuongezeka siku hadi siku toka asilimia 50 mwanzo wa mwaka 2015 hadi asilimia97 mwaka huu.

Naye Afisa elimu wilaya ya Mkuranga Ndg. Cosmas Magige akichangia katika mkutano huo alipendekeza kufanyike jitahada za kuwapikia wanafunzi lishe hiyo shuleni ili kuimarisha afya zao na kupunguza utoro shuleni.

Kwa upande wake Afisa lishe wilaya Bi. Vumilia alisisitiza matumizi ya viazi lishe kwa wakazi wa wilaya hiyo ikiwa ni mpango wakupunguza tatizo la upungufu wa damu kwa wagonjwa wanaohudhuria tiba katika zahanati mbalimbali kwani takwimu zinaonesha asilimia 70 ya watu wanaopimwa hukutwana upungufu wa damu hivyo msisitizo katika ulaji wa viazi lishe pamoja na majani yake itakua suluhu ya tatizo hilo badala ya uchangiaji damu ambao una changamoto nyingi mpaka sasa.

Mwenyekiti wa kamati ya Uchumi wilaya na diwani wa kata ya Tengelea Mh.Shaban Manda alisema wapo tayari kuongeza nguvu katika kuelimisha jamii ili kuunga mkono juhudi za kuimarisha afya na kipato kutokana na zao hilo.

Mmoja ya wakulima waliofanikiwa kulima zao hilo, Festus Sebastian amezungumzia faida aliyoipata kutoka na na zao hilo “viazi lishe vinatoa viazi vingi sana na tangu nimeanza kilimo hiki nimeshagawa mbegu kwa wakulima 20 kama mradi unavyotaka”

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.