• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

DED MKURANGA AWAFUNDA WATENDAJI KUSIMAMIA MIRADI

Posted on: July 22nd, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Waziri Kombo amesema haridhishwi na kiwango cha usimamizi na utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo.

Kauli hiyo ameitoa katika kikao kazi kilichofanyika Julai 22, 2025 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga.

Kombo amesema ataendelea kuchukua hatua kali kwa mtumishi atakayesababisha kucheleweshwa kwa mradi au kusababisha mradi huo kutofanyika vizuri, na kwa msisitizo tayari ameanza kuchukua hatua kwa watumishi kadhaa mpaka sasa.

Amesema kwa mwaka huu anataka kila mtumishi akae katika kituo chake cha kazi sambamba na kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizopo ili kutoa huduma zilizo bora kabisa.

Sambamba na hayo, amesema hatowavumilia watumishi kuanzia ngazi ya Kata mpaka Kijiji ambao katika maeneo yao Miradi ya Maendeleo haitekelezeki vizuri na kushindwa kumalizika kwa wakati.

Aidha akizungumzia suala la mapato Mkurugenzi amesema ni suala mtambuka hivyo kila mmoja anatakiwa kuwajibika na kuhakikisha Serikali inakusanya mapato vizuri.

Kwa upande wake Mtendaji wa Kijiji cha Mkuranga Juma Diffa kwa niaba ya watendaji wenzake amemshukuru Mkurugenzi kwa kutoa maelekezo hayo na kuahidi kuwa na utekelezaji mzuri katika majukumu yao.

Kikao hicho kilichowakutanisha Watendaji wa Kata na Vijiji, Waganga Wafawidhi pamoja na Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari kilikuwa na lengo la kujadili umuhimu wa kukusanya mapato na kuhakikisha Miradi ya Maendeleo inakamilika kwa wakati kulingana na fedha zinazotolewa.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • DED MKURANGA AWAFUNDA WATENDAJI KUSIMAMIA MIRADI

    July 22, 2025
  • SILAA AELEKEZA TCRA KUFIKA RADDY FIBER MKURANGA

    June 18, 2025
  • RC KUNENGE AIPONGEZA MKURANGA KUPATA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • UWT YAZINDUA KAMPENI YA UTOAJI ELIMU ILANI YA CCM

    June 11, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.