• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Elimu ya Lishe kuanza kutolewa kuanzia ngazi ya familia Mkuranga

Posted on: December 18th, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga imejipanga kukabiliana na tatizo la lishe duni kwa kuongeza uelewa wa masuala ya lishe katika jamii, kuanzia ngazi ya familia hadi kwa watendaji na viongozi

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala Wilaya ya Mkuranga, Bi. Dalmia Mikaya kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, wakati wa Mafunzo ya Maandalizi ya Mipango na Bajeti ya Lishe katika Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2020/2021, yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa mkuu wa wilaya na kushirikisha viongozi, wataalam na wadau mbalimbali wa masuala ya lishe

Aliongeza kuwa, hali ya lishe ya jamii sio ya kuridhisha, kwani takwimu zinaonesha kwa Mkuranga tatizo la upungufu wa damu kwa watoto ni 50.2%, uzito pungufu 24%, Udumavu ni 16%, Ukondefu ni 7%, huku kwa mwaka 2017 pekee 90%  ya vifo vinavyotokana na uzazi vilitokana na upungufu wa damu. pia akaainisha mikakati kwa jamii ya Mkuranga kuwa ni kutoa elimu ya lishe kwa kupitia mikutano ya hadhara ya kiserikali, maonesho kwa sinema, michezo ya jadi, mashindano mbalimbali, mabango, vipeperushi n.k. na kutaka suala la lishe kuwa agenda mtambuka katika vikao vyote vya Halmashauri.  Mwisho akizitaja kata zinazoongoza kwa kuwa na wagonjwa wengi wa utapiamlo kuwa ni Kimanzichana, Vikindu, Mkuranga, Kisiju, Bupu, Tengelea, Njianne, Lukanga, Kiparanganda, na Mwarusembe kuwa zitapewa kipaumbele cha mradi wa kutokomeza utapiamlo.

Kwa upande wake Mwezeshaji wa Mipango na bajeti toka  Ofisi ya Rais Tamisemi  Bwn. Mkama Dickson Lugina, alisisitiza wadau wa masuala ya lishe kuendelea kutoa elimu ya lishe kwa jamii hususani kuzingatia umuhimu wa lishe katika siku 1000 za mtoto (tangu siku ya kutungwa kwa mimba) kuwa ndio muhimu zaidi katika kumjenga mtoto kiafya na kiakili na kumuepusha na udumavu.

Aidha alieleza mambo ya kuzingatia ili kuwa na lishe bora kuwa ni pamoja na Umuhimu wa kumnyonyesha mtoto (zaidi katika miezi 6 ya mwanzo baada ya kuzaliwa), Umuhimu wa chakula cha nyongeza, Utoaji wa vitamin A, Kupambana na ongezeka la wanawake wenye uzito mkubwa na viriba tumbo, Utumiaji wa madini joto, Makuzi changamshi na Kusisitiza umuhimu fedha za bajeti za vituo (DHFF) kupelekwa mojakwamoja kwenye vituo kwa ajili ya shughuli zenye matokeo makubwa

Naye, Afisa Lishe (M) Bi. Pamela Meena akichangia katika Mafunzo hayo ilisema, pamoja na changamoto nyingi katika kukabiliana na lishe duni, moja ya changamoto kubwa ni kutokuwepo kwa mikakati shirikishi kwa idara zote katika Halmashauri Hivyo Kuagiza kila idara kupendekeza na kuandaa Sampuli ya shughuli ambazo zitawekwa katika Mipango na bajeti za lishe katika halmashauri hiyo

Katibu Tawala Wilaya ya Mkuranga Bi. Dalmia Mikaya akihutibia wakati wa ufunuzi wa mafunzo hayo. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Eng: Mshamu Munde



Mwezeshaji wa Mipango na Bajeti za Lishe kwa Halmashauri na Mkoa, Bi. Emma Vicent Kilimali akitoa maelezo katika vikundi wakati wa mafunzo hayo 




Mshiriki wa mafunzo hayo akitoa mipango mikakati ya Idara mbalimbali za Halmashauri kwa ajili ya Mipango na Bajeti ya Halmashauri kwa mwaka 2020 / 2021


Mwezeshaji Mipango na Bajeti toka Ofisi ya Rais Tamisemi, Bw. Mkama Jackson Lugina akitoa mada wakati wa mafunzo




Wasiriki na wawezeshaji wa semina hiyo katika picha ya pamoja na viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga



Pamela Meena, Afisa Lishe Mkoa wa Pwani akitolea ufafanuzi moja ya hoja zilizotolewa na mshiriki wa mafunzo hayo 

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.