Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

HALMASHAURI YA MKURANGA WAUNGANA NA LUKUVI

Posted on: September 15th, 2019

WANANCHI wa vijiji vinavyounda Wilaya ya Mkuranga  Mkoa wa Pwani  wameamua kuunda kamati  za kuhamasisha na kufatilia fursa ya urasimishaji ardhi hatimaye waweze kupata hati ya umiliki iweze kuwasaidia kwenye masuala mbalimbali ikiwemo mikopo katika taasisi za fedha

Akizindua zoezi la upimaji na umilikishaji ardhi kwenye kijiji cha marogoro juzi, Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya Mkuranga Mhandisi Mshamu Munde aliwapongeza wananchi wa vijiji vya Mfuru mwambao,Yavayava,na Marogoro kwa mwamko wao wa kulipia Halmashauri sh.laki na nusu kila mmoja za urasimishaji huku akiviagiza vijiji vingine vichangamkie fusra hiyo ambayo imeletwa na serikali  ya awamu ya tano inayoongozwa na Raisi Dkt.John Pombe Magufuli 

Munde aliwataka wananchi hao wanaozidi 100 watumie muda huu kabla septemba 29 mwaka huu ambapo wataalamu wa ardhi wataanza kupima na kumilikisha wasafishe maeneo yao, wajaze fomu maalumu yenye nakala ya malipo ya benki ili kuepuka  migongano.

Kwa upande wake Afisa  ardhi mteule   wa Halmashauri ya Wilaya Musa Kichumu alisema wameamua kutekeleza maagizo ya Waziri wa ardhi, nyumba, na maendeleo  ya makazi  William Lukuvi kuwatoza wananchi hao laki na nusu huku wakizingatia kutenga  barabara  za mitaa maeneo ya huduma za jamii yakiwemo ya kuzikia

Naye Diwani wa kata ya vianzi yenye mradi huo Nassoro Chuma  alimpongeza  Mkurugenzi Munde kwa kushughulikia mapema mchakato huo wa urasimishaji  kwa wananchi wake  huku akiwaagiza watendaji wa vijiji vya kata hiyo wahamasishe wananchi wafaidike na mpango huo sambamba na kuwa nao bega kwa bega  wataalamu  wa ardhi katika upimaji na umilikishaji

Akitoa neno la shukrani katibu wa kamati ndogo ya mipango miji ambaye pia ni mnufaika  Twahil Shabani “kamona” alimwomba Mkurugenzi Munde awasiliane na meneja wa (TARURA) Wilaya Mhandisi Peter Shirima ili akarabati barabara ya vikindu hadi sangatini iwe rahisi kusafirisha vifaa vya ujenzi maeneo yao.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • RO MKURANGA AWAFUNDA WAANDIKISHAJI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI

    May 14, 2025
  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.