• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

kata 14 zapatiwa elimu ya uhaulishaji Mkuranga

Posted on: March 26th, 2018

Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga imetoa mafunzo ya uhamasishaji wa wataalamu ya namna ya kutekeleza majukumu yao ili kufanikisha mpango wa uhaulishaji katika kata 14 mwanzoni mwa mwezi machi 2018.

Akizunguzumza wakati wa uhamasishaji huo katika kata ya Mkuranga Mratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF) bwana  Timoth Kudra alisema kata ambazo zimeshafanya vikao vya uhamasishaji ni kata 14 kati ya 18 ambazo ni Mkuranga,Vikindu,Kiparang’anda,Shungubweni,Mbezi,Kisiju,Magawa,Lukanga,Njianne,Mkamba,Bupu,Kimanzichana,Panzuo na Nyamato.

Mratibu huyo aliongeza kwamba lengo la uhamasishaji huu ni kuwajengea uwezo watendaji wa kata,Maofisa Maendeleo ya Jamii,Maofisa Ustawi wa Jamii,Watendaji wa Vijiji ambavyo mpango upo, Walimu Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari pamoja na waganga wafawidhi wa vituo vya afya na zahanati.

Bi Zubeda Mkupeta Afisa Afya  alisema kikao cha  uhamasishaji kimemsaidia kujua vema majukumu yake katika mradi huu ambapo anatakiwa kuhakikisha anadhibiti kinga kwa watoto wa umri wa 0-5 na kuhakikisha watoto wote wanapata chanjo na kuhudhuria kliniki kwa wakati  stahiki pia kuhamasisha kaya zote kujiunga na Mfuko wa afya ya jamii(CHF).

Bwana Ame Mnyanga Afisa Mtendaaji wa kata ya Panzuo alisema kikao cha uhamasishaji kimemsaidia kufahamu zaidi kuhusu mradi wa TASAF na malengo yake makuu ya kuweza kuwajengea uwezo kaya maskini na kwenda kwenye hali nzuri ya maisha.

Mnyanga aliendelea kusema watendaji wa kata, vijiji na wataalam wengine wamefanikiwa kutambua kwa urahisi majukumu yao na hivyo kuwapelekea kufanya kazi kwa bidii na kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Tasaf awamu ya tatu-Mpango wa kunususru kaya maskini unawezesha kaya maskini kupata mahitaji ya msingi, kulinda rasilimali zao na kuweka akiba kwa ajili ya kujiletea maendeleo na hatimae kujitoa kwenye umaskini.

Madhumuni ya TASAF awamu ya tatu ni kuziwezesha kaya kupata mahitaji ya msingi na fursa za kujiongezea kipato.Walengwa wa mpango ni kaya maskini katika maeneo yaliyoainishwa.Maeneo yaliyotiliwa mkazo ni kunusuru kaya maskini kwa kuzipatia fedha ambazo zitasaidia kwenye uzalishaji mali ili wapate manufaa ya muda mrefu,pia kutoa ajira za muda mfupi kwa walengwa wenye uwezo wa kufanya kazi kutoka kwenye kaya maskini na kuzipatia ustadi mbalimbali, pia kukuza na kuchochea utamaduni wa kaya maskini kujiwekea akiba na kuzipa elimu ya masuala ya fedha na uendeshaji wa biashara ndogondogo, pia kuwezesha jamii maskini kujenga/kuboresha miundo mbinu ya maji, elimu na afya katika maeneo ambayo hayana huduma hizi ili walengwa wapate huduma hizi ikiwa ni kigezo cha kutimiza masharti ya mpango

Wilaya ya mkuranga ina kaya 51,101 kwa mujibu wa sensa ya mwaka  2012 na TASAF ime wezesha kaya 4690 kwa vijiji 77 kati ya 125.Mpango huu ulizinduliwa septemba 2014 na utekelezaji wake ulianza julai 2013.Mpaka kufika februari 2018 Wilaya ya Mkuranga imetumia jumla ya Tshs 2,828,156,000 katika zoezi la uhaulishaji katika kaya maskini.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.