• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mafunzo ya uokaji wa bidhaa zinazotokana na unga wa muhogo

Posted on: August 25th, 2017


Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga ikishirikiana na Cassava Adding Value for Africa (CAVA) wametoa mafunzo ya siku mbili yanayohusiana na  uokaji bidhaaa zinazotokana na unga wa muhogo.Mafunzo hayo yalifanyika Wilayani Mkuranga kuanzia tarehe 23-24/05/2017 ambapo yalijumuisha washiriki 64,wanawake 48 na wanaume 16 kwenye ukumbi wa upashanaji habari kiguza ikiwahusisha wakulima na wajasiriamali kutoka maeneo mbalimbali ndani ya Wilaya ya Mkuranga.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo meneja wa mradi wa CAVA bi Grace Mahende alisema lengo la mafunzo hayo ni kuongeza kipato kwa wajasiriamali ili kuweza kuwapatia masoko zaidi hususani soko la muhogo mbichi na mkavu.

Grace aliongeza kwamba”wajasiriamali wanatakiwa wasimame kwenye nafasi yao,kwasababu ni muhimu katika kufungua masoko, mahitaji yataongezeka na kipato pia kitaongezeka”alisema

Aidha bi Grace alishauri wakulima watumie unga bora wa muhogo kwani sio  kila unga wa muhogo unatoa bidhaa bora,alisema ili kupata bidhaa nzuri za unga wa muhogo watumie chipper machine na sio unga wa makopa.

 Dosa Deus Mkazi wa Mwarusembe anajishughulisha na kilimo cha muhogo na ufugaji ni miongoni mwa washiriki wa mafunzo ya uokaji bidhaa zinazotokana na unga wa muhogo alisema”Nimehamasika  sana kuja kwenye mafunzo kwasababu mimi ni mkulima wa zao la muhogo hivyo nimepata mafunzo namna ya kuongeza thamani kwenye zao la muhogo na sasa nimeelewa namna ya kutengeneza bidhaa mbalimbali kama kupika tambi hivyo nikitoka hapa nitatengeneza tambi na kuuza hata hivyo utengenezaji wake ni rahisi zaidi”

Bi Sophia Robert Mkazi wa Mkuranga mjini  ambaye anajishughulisha na  ujasiriamali alisema mafunzo aliyoyapata atayafanyia kazi kwa vitendo kwa kupika  maandazi, kripsi na tambi na kuweka kwenye genge lake ili kujiongezea kipato.

Bi Janeth Mbwambo Meneja wa Mkuranga Cassava Cooperative Joint Enterprises (MKUCACOJE) alisema  mafunzo haya yalikuja baada ya kuuza unga wa muhogo kwa watu mbalimbali na walipoona malekezo ya  namna mbalimbali jinsi  unga huo  unavyotumika kutengeneza bidhaa mbalimbali wananchi hao waliomba wafundishwa namna ya kupika bidhaa hizo.

Akifafanua zaidi Janeth alisema baada ya kuona mahitaji hayo aliwasiliana na Meneja wa  CAVA na ombi hilo likakubalika na wamegharamia mafunzo hayo kwa kununua mahitaji mbalimbali ikisaidiana na Halmashauri ya Wilaya.

CAVA inashirikiana na wadau mbalimbali wa mnyororo wa thamani wa zao  muhogo wakiwemo wakulima, wasindikaji na watumiaji pamoja na watoa taaluma katika nchi tano za Afrika ikiwemo Tanzania,Malawi,Uganda,Nigeria na Ghana. Mradi huu ni wa miaka mitano na sasa hivi ni awamu ya pili tangu ulipoanza mwaka 2014 na unatarajia kumalizika 2019.


Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.