• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Migogoro itatuliwe na Watendaji ngazi za kata-DED Munde

Posted on: April 18th, 2018


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Mhandisi Mshamu Munde amewataka watendaji katika ngazi za kata kutatua migogoro mbalimbali ili kuepusha wananchi wengi kufika Ofisi ya Mkurugenzi kwa lengo la kusaidiwa kutatuliwa migogoro hiyo.

Munde aliyasema hayo hapo jana wakati wa kikao kazi kilichofanyika kwenye ukumbi wa Parapanda ambapo kikao hicho kiliwajumuisha watendaji wote katika ngazi za kata wakiwemo Maofisa Kilimo, Maofisa Mifugo na Uvuvi,Maofisa Ustawi wa Jamii,Maofisa Maendeleo ya Jamii na Waratibu Elimu kata.

Munde aliongeza kwamba migogoro mingi huanzia  kwenye  ngazi zavijiji na kata hivyo ni rahisi watendaji kwenye ngazi husika kujihusisha kutatua migogoro hiyo kuliko kuacha wananchi hao kufika kwenye ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kusaidiwa kutatuliwa migogoro yao wakati kwenye ngazi ya kijiji wanafahamu migogoro hiyo kwa undani zaidi.

Munde alisisitiza kwamba Serikali huanzia kwenye ngazi za vijiji hivyo watendaji kwenye ngazi hizo  wahakikishe wanawaaminisha wananchi wao kuhusu  utendaji wao ili migogoro inayoletwa kwenye ofisi yake ipungue.

Afisa maendeleo ya Jamii Wilaya Bwana Peter Nambunga ambaye pia alikuwa mratibu wa kikao kazi hicho  alisema lengo kubwa la kuwaita watendaji kwenye ngazi za kata ni kuongeza usimamizi, uwajibikaji, ufuatiliaji na upatikanaji wa taarifa kwa ngazi za chini ili kupunguza majukumu na ufatiliaji kwa Mkurugenzi Mtendaji na Mkuu wa Wilaya kwani itajenga ufahamu wa kufanya kazi pamoja kisekta.

Nambunga aliongeza kwamba wanatarajia kikao kazi hiki kitasaidia kupunguza changamoto mbalimbali za wananchi kupitia mamlaka zao kwa kutoa maelekezo kwa wananchi jinsi gani wanaweza kutatua matatizo katika mamlaka zao za vijiji na kata kabla ya kufika kwa Mkurugenzi Mtendaji au Mkuu wa Wilaya sambamba na kufahamu changamoto wanazokutana nazo katika utekelezaji wa majukumu yao ya kazi na namna ya kuzitatua changamoto hizo.

Afisa Mtendaji kata ya Kisiju bwana Juma Katundu alishukuru sana kwa kufanyika kwa kikao kazi hicho na kusema kwamba kimewasaidia kutambua umuhimu wa  kufanya kazi kwa ushirikiano katika ngazi za kata lakini pia watendaji wote katika ngazi za kata watakua wanaongea lugha moja katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Wataalamu hao wamejiwekea mikakati mbalimbali katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na pia kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili ili kufikia lengo la utoaji huduma bora kwa wananchi kwa kufanya vikao kazi hivyo kila  baada ya miezi minne.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.