• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

MITI IPANDWE KUPAMBANA NAMABADILIKO YA TABIA NCHI....

Posted on: April 15th, 2021

Mkuu waWilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani Mh. Filberto Sanga amewataka wananchi kujenga tabia ya kupanda miti katika maeneo wanayoishi ili kuepusha madhara makubwa yanayoweza kusababishwa na uharibifu wa mazingira kutokana na mabadiliko ya hali ya tabia Nchi

Sanga aliyasema hayo wakati akihutubia hadhara katika viwanja vya shule ya msingi chatembo wakati wa maadhimisho ya siku ya upandaji miti ambapo alisema hili ni agizo linalotekelezwa kutokana na waraka uliotolewa na Serikali wa  kuwataka wanachi wote kushiriki siku ya upandaji miti kitaifa kila mwaka ili kupunguza madhara yanayotokana na uvunaji wa miti kwa ajili ya shughuli za binadamu .

“Maamuzi ya kupanda miti kila mwaka yamefikiwa baada ya kuona misitu katika nchi yetu inatoweka kutokana na shughuli za kila siku za kibinadamu hasa matumizi yanayozidi uwezo wa misitu yetu kujizalisha hali hii imesababisha maeneo mengi kupata athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo joto, mafuriko, vimbunga” alisema.

 Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya Mhandisi Mshamu Munde alisema kwa taarifa iliyopo utendaji wetu  sio mbaya kwa kuwa vitalu vya vikindu na kibiti vinasaidia kwenye kutimiza malengo hayo ya kuzalisha miche mbalimbali ya miti

Sambamba na hilo, Munde alisema “natambua pia kuna changamoto za wananchi wa kawaida kutojihusisha na upandaji wa miti hususani isiyokuwa ya matunda” 

Aidha, aliendelea kusema kuwa umuhimu wa misitu ni mkubwa sana sisi kama Wilaya tumejipambanua kwa sababu tuna viwanda vingi sana lakini shughuli za viwanda zinaenda Pamoja na uzalishaji wa hewa taka na sio tu kwa sababu ya shughuli zao lakini ni Pamoja na uwingi wa watu wanaofanya kazi katika viwanda hivyo, hivyo basi ni muhimu kuendelea kupanda miti ili kusaidia kurekebisha hali ya hewa  na kupunguza athari za hewa chafu inayotokana na uwepo wa viwanda.

Katika maadhimisho hayo watu binafsi na Taasisi mbalimbali vimehamasishwa kutumia fursa iliyotolewa na mfuko wa misitu Tanzania (TaFF) kuandika miradi ya hifadhi za misitu na ufugaji wa nyuki na kuwezeshwa.

Msitu wa Vikindu,kwa sasa unatumika kuingiza kipato kwa shughuli za utalii ikologia, ambapo  watalii 161 wa ndani na wa nje wametembelea kivutio hiki kilichokuwa kichaka cha kujificha wahalifu na eneo la uvunaji haramu wa mazao ya misitu.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.