• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

MKURANGA KUPATA NEEMA

Posted on: September 17th, 2021


Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga imehakikishiwa kujengwa kwa Kituo kikuu cha Mabasi yaendayo kusini na Nchi jirani kusini mwa Tanzania katika Kijiji cha Kipala Mpakani kata ya Mwandege na wananchi wa Mkuranga wamekubaliana kukiita kituo hiko kwa jina la “kituo cha mabasi cha Samia Suluhu Hassan”.

Hayo yamesemwa mwishoni mwa juma lililopita  katika mkutano wa wananchi waliokuwa katika kijiji cha Tambani na waziri wa nchi ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Ummy Mwalimu katika ziara ya kukagua miradi ya Afya, Elimu na Miundo mbinu wilayani Mkuranga,ambapo katika suala la elimu bure kwa shule za msingi na sekondari litaendelea kuwepo na kuwataka wananchi kupuuza taarifa za watu zinazoendelea za kusema Elimu bure inaenda kufa.

Waziri Ummy ameongeza kuwa sambamba na hilo ataongea na viongozi wa DART ili kuona ni namna gani wataweza kufanikisha barabara ya mwendo kasi inafika vikindu kwa lengo la kuifanya Mkuranga kupata huduma bora kulingana na wananchi wengi wanaohamia kwa wingi ndani ya wilaya hiyo.

Aidha Ummy Mwalimu amewahakikishia wananchi wa Mkuranga kuwa Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imekusudia kujenga shule moja ya Sekondari kila Kata sambamba na kumtaka Mkandarasi anayejenga daraja la Mipeko linalogharimu kiasi cha shilingi milioni 200 kumaliza kazi hiyo katika muda uliopangwa.

Nae mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari kunenge amemuhakikishia wao kama Mkoa watajipanga na watashirikiana vema na viongozi wa wilaya ili kuhakikisha fedha zote za Miradi zinasimamiwa vema na watafanya kazi kwa lengo la kuleta maendeleo chanya kwa wananchi wa Mkoa wa Pwani.

Awali akiwasilisha maombi ya Wilaya hiyo Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega allimuomba Waziri kuwasaidia wananchi wa Mkuranga mambo matatu, ujenzi wa Kituo cha Mabasi yanayokwenda kusini mwa Tanzania, miundo mbinu ya Barabara na Madaraja pamoja na kuiboresha hospitali ya Wilaya ambapo Tayari waziri amesema iko haja ya kujenga hospitali mpya ya wilaya na ile iliyopo itumike kama kituo cha afya.

Akitoa nenO la shukrani Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Mwamtumu Mgonja amemuahidi waziri kwa niaba ya Rais wao kama Halmashauri watashirikiana kwa kiasi kikubwa katika kukusanya na kuongeza mapato ili kuleta  maendeleo kwa wananchi wa Mkuranga.

Madiwani wametakiwa kumuunga Mkono Rais katika jitihada zake za kuleta maendeleo nchini sambamba na kuacha kulumbana na kutakiwa kushirikiana katika kusimamia miradi ya maendeleo.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.