• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mkuranga wampongeza Mama Janet Magufuli

Posted on: March 8th, 2020

Mke wa Rais mama Janet Magufuli amepongezwa  na wananchi wa Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani kufuatia huruma yake kwa watoto wenye ulemavu baada ya kutoa msaada wa baiskeli maalum kumi ambazo zitawasaidia baadhi ya watoto hao wenye ulemavu.

Akizungumza na wananchi katika kilele cha kusheherekea Sikukuu ya Wanawake Duniani iliyofanyika Kiwilaya kwenye Kijiji cha Kisemvule jana,  Mbunge wa Jimbo la Mkuranga ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mifugo na uvuvi  Abdallah Ulega amesema msaada huo aliokabidhiwa  Ikulu ndogo Jijini Dar Es Salaam wiki iliyopita ni kielelezo tosha ni jinsi gani Rais Dr. John Pombe Magufuli na mkewe walivyo na mapenzi ya dhati kwa wananchi wa Mkuranga.

Katika sherehe hizo Ulega alimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Mhandisi Mshamu Munde awasimamie watendaji na wataalam wa Kata zote (25) waandae Miradi ya Kimkakati katika sekta mbalimbali hatimaye shilingi Milioni (500.6) zilizotengwa na Halmashauri kwa ajili ya Mikopo ya Wanawake, Vijana na Walemavu zinaleta tija kwa wananchi.

Aidha Mbunge huyo alilipongeza Jukwaa la Wanawake Wilaya ya Mkuranga  kwa uwezeshaji kiuchumi kwa kuwa na mikakati ya kuwakwamua wanawake kwa kuviwezesha vikundi Vijijini  huku akiwaahidi kuandaa Semina ya kuwajengea uwezo, kuwapa Mifugo ya Kuku na kuwapa Vyerahani (25) katika Kata zote.

Akizungumzia Miradi ya Maendeleo, Ulega alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais Magufuli kwa kuipa Halmashauri hiyo mamilioni ya pesa katika Miradi ya Barabara, Umeme, Maji, Elimu na Afya huku akiwaomba wananchi  kuonyesha shukrani katika Uchaguzi Mkuu ujao kwa kuchagua Rais, Mbunga na Madiwani kupia Chama cha Mapinduzi (CCM).

Awali Mwenyekiti wa jukwaa hilo Mariamu Ulega, aliiomba Serikali kuangalia kwa karibu kundi la Wanawake kwa kuwaongezea Mikopo ili waweze kujikwamua kiuchumi huku akiwahakikishia wanawake wenzake kuandaa harambee itakayowashirikisha wadau mbalimbali hatimaye Jukwaa hilo liweze kuendesha miradi ya wanawake kikamilifu.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Mkoa, Wilaya na Kata, ilifungwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Kisemvule Omari Makunge kwa kuwaomba  wananchi kutunza Miradi iliyopo katika Vijiji vyao  ili iwe endelevu sambamba na kujitokeza kwa wingi katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.