• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mkuranga waomba Walimu kwa Waziri

Posted on: August 15th, 2017


Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani imeomba serikali kuongeza idadai ya walimu wa masomo ya sayansi  ili kuboresha elimu katika wilaya hiyo na kunusuru shule za Wilaya hizo dhidi ya matokeo mabaya ya kidato cha nne.

Akisoma risala mbele ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia  Mh.Prof.Joyce Ndalichako,Afisa Elimu Sekondari Wilaya Bwana Benjamin Majoya alisema kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi  kujiunga na elimu ya Sekondari jambo ambalo limesababisha uhitaji wa walimu mkubwa.

Alisema kwa sasa wilaya ya Mkuranga ina uhaba wa walimu 485 ikilinganishwa na idadi ya 1642 ambapo wanahitajika ili kutosheleza mahitaji.

“kwa kiasi kikubwa uhitaji wa walimu ni kwa upande wa masomo ya sayansi ambapo tunahitaji walimu 77” alisema bwana Majoya.

Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Mh.Juma Abeid ameiomba Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  kufanya mawasiliano na Halmashauri ili kujua uhitaji wa walimu katika shule wilayani humo badala ya kugawa walimu katika maeneo yalio na idadi kubwa ya walimu huku kukiwa na maeneo yenye idadi ndogo  ya walimu.

Akizungumza mbele ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Prof.Joyce Ndalichako Mh Abeid alisema licha ya kuwepo kwa uhitaji wa walimu bado idadi ya walimu wanaoletwa katika wiaya hiyo huwa wanaelekezwa kwenye vituo vyenye utoshelevu.

“Tatizo hili ni kikwazo tena si katika elimu tu pia afya ambako kuna zahanati zina muhudumu mmoja  mmoja wakati kuna maeneo mengine yana uhitaji mkubwa”Alisema

Mbunge wa Mkuranga Mh Abdallah Ulega  akizungumza mbele ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof Joyce Ndalichako alisema Wilaya ya Mkuranga ni miongoni mwa maeneo nchini ambayo yana mwamko mdogo wa elimu huku kukiwa na idadi kubwa ya wahitimu ambao hawakufanya  vizuri kwenye mitihani yao ya Kumaliza elimu ya sekondari  na hivyo kutoendelea na masomo.

Mbunge huyo amemuomba Waziri Ndalichako kutimiza adhma ya muda mrefu ya wananchi wa Mkuranga  kwa kusaidia  ujenzi wa Chuo cha Mafunzo ya Ufundi (VETA) ili kuzalisha wataalamu wengi katika kueleka nchi ya viwanda.

“kwa kipindi kirefu Baraza la Madiwani liliazimia  na tukaandaa  eneo  kwa ajili ya ujenzi,hatutapenda kuona vijana wetu wanaenda kuwa manamba katika viwanda ambavyo vinaendelea kujengwa na kuboreshwa kila kukicha “Alisema

Aidha Waziri Ndalichako amewataka uongozi wa Wilaya  hiyo inafanya jitihada  na kuhakikisha  kiwango cha ufaulu kinapanda katika wilaya hiyo ili kuunga  mkono jitihada za Serikali  ambayo inatoa fedha za elimu kila mwezi.

“Jitihada hizi zianze  mwaka huu ili tupate matokeo mazuri ya mitihani inayofanyika mwaka huu kwani muda upo wa kufanya mabadiliko na kuleta matokeo chanya” alisema.

Alisema ni jambo la muhimu kwa wananchi kutambua jitihada za serikali inayotoa bilioni 17.7 kila mwezi kwa ajili ya kufanikisha  elimu bure.


Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.