• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mkuranga Wapata Suluhisho la Maji

Posted on: October 15th, 2017

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe ameahidi kutatua changamoto ya maji eneo la Mkuranga mjini  Mkoani  Pwani.

Waziri huyo aliyasema  hayo hapo jana wakati alipofanya kikao na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Uongozi wa Chama cha Mapinduzi na Wakuu wa idara mbalimbali baada ya kuona changamoto ya upatikanaji wa maji mjini Mkuranga.

Akisoma Taarifa ya huduma ya maji Wilaya Mhandisi Renard Baseki alisema  huduma ya maji wilayani hapa maeneo ya vijijini yamekuwa yakipata maji kwa wastani wa asilimia 62.5 na huduma hii hutolewa kwa kutumia miundombinu ya maji ya mitandao ya bomba, visima virefu na vifupi vya pampu za mkono na zinazoendeshwa na mitambo ya jenereta za nishati ya mafuta, umeme wa mguvu ya jua na mifumo ya kuvuna maji ya mvua.

Aidha Baseki aliendelea kufafanua kwamba jumla ya wakazi 2512 wa makao makuu ya Halmashauri ya Mkuranga wamekuwa wakipata maji safi na salama sawa na asilimia 10 ya wakazi wote  wa mji.kijiji hiki hupata maji kutoka katika chanzo ambacho ni kisima kirefu kilichopo eneo la kulungu.

Mhandisi Mshamu Munde Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga alisema” Tuna tatizo kubwa la upatikanaji wa maji hapa mjini Mkuranga, malalamiko kwa wananchi ni mengi sana hivyo tukipata fungu la kutengeneza miundombinu ya maji tutakuwa tumetimiza kiu ya wananchi wetu”

Kufuatia changamoto hiyo Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mh Mhandisi Isack Kamwelwe alisema “Mniandikie andiko kwa ajili ya kutatua changamoto hii na andikeni hilo andiko bila kujali bajeti yenu  ili nilifanyie kazi”.

Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mh Filberto Sanga aliongeza kwa kusema Wilaya ya Mkuranga ina maji mengi ardhini ambayo ni safi na  salama hata viwanda vyote vya Mkuranga hutumia maji hayo kwa matumizi ya viwanda na alimuhakikishia Waziri wa Maji na Umwagiliaji kuandika andiko hilo ili kutatua changamoto ya maji mjini Mkuranga na kupeleka ofisi ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji.

Wilaya ya Mkuranga ina vyanzo vikuu mbalimbali ikiwa ni pamoja na uvunaji wa maji ya mvua, maji ya chini ya ardhi(Underground Water), Chemichemi na mabwawa. Mpaka juni 2017 jumla ya wakazi 123,623 wanapata huduma ya maji safi na salama, hii ni sawa na asilimia 62.5 ya wakazi wote 197,797 wa Mkuranga waishio vijijini. Vilevile asilimia 10 ya wakazi wa mji wa Mkuranga ndio wanaopata huduma ya maji safi na salama.


Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.