• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Naibu waziri aipongeza Raddy Fibre kuwekeza sekta ya mawasiliano

Posted on: February 26th, 2021


NAIBU Waziri wa Mawasiliano na TEHAMA, Mhandisi Kundo Mathew, amekipongeza Kiwanda cha Raddy Fibre Solution kilichopo Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani kwa kuwekeza kwenye sekta ya mawasiliano.

Akizungumza na wananchi wa Wilaya hiyo juzi baada ya kukagua uzalishaji wa bidhaa za Mkongo wa Taifa unaofungwa na kiwanda hicho cha wazawa, Kundo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bariadi, alisema uwekezaji huo uliogharimu sh.bilioni 1.7 utafanikisha ujenzi wa mkongo wa Taifa upungue gharama na kuokoa fedha za kigeni.

Mhandisi huyo alizitaka Idara za Uhamiaji na Zimamoto kutoa ushirikiano kwa wawekezaji hao ili waweze kutimiza malengo yao kwani kiwanda hicho kitatoa ajira zisizopungua 400 sambamba na kuongeza mapato ya Halmashauri ya Wilaya na Serikali Kuu.

Akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Ramadhani Mlanzi, aliipongeza Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwezesha kuanza ujenzi, huku akiweka bayana azma yake ya kutengezeza cable za fibre kilometa 24 elfu kwa mwaka na kuongeza wao ni kati ya nchi tatu pekee za Afrika zinazofanya uzalishaji huo.

Katika taarifa ya Halmashauri hiyo iliyosomwa na Mkurugenzi, Mhandisi Mshamu Munde ilisema mazingira rafiki kwa uwekezaji ikiwemo ardhi ya kutosha imewavuta zaidi ya wawekezaji 80 hali iliyochangia kutoa ajira kwa wananchi na kupaisha mapato.

Akiwasilisha taarifa ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (USCSAF) Mkuu wa uendeshaji Albert Richard alisema wametumia sh.bilioni 161 za serikali kujenga mikongo kwenye Kata 1057 nchini huku Wilaya ya Mkuranga wakitumia milioni 200, ambapo Naibu Waziri aliridhika na usikivu baada ya kukagua.

Akitoa neno la shukrani, Mkuu wa Wilaya hiyo, Filberto Sanga aliwataka wajenzi wa mikongo kutoa taarifa kabla kwa Mkurugenzi, Uongozi wa Kata na Vijiji ili kujiridhisha zaidi kiusalama.


Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.