• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Naibu Waziri wa Afya awataka wananchi kuepuka magonjwa yasiyoambukizwa

Posted on: October 31st, 2017


Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mh.Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile amewataka wananchi kuepuka magonjwa yasiyoambukizwa kwa kufanya Mazoezi, kula Lishe bora,kuepuka matumizi ya pombe kupita kiasi na matumizi ya tumbaku.

Dkt Ndugulile aliyasema hayo hapo Jana wakati wa ufunguzi wa huduma ya Macho,Kisukari na Shinikizo la damu Wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani ambapo huduma hiyo ilifadhiliwa na Lions Club ya Dar es Salaam,Kiwanda cha Knauf Gypsum Ltd kilichopo Mkuranga na Hospitali ya Regency iliyopo Dar es Salaam ambapo huduma hiyo ya matibabu ya bure ilianza tarehe 27.10.2017 na inatarajia kumalizika Leo hii tarehe 29.10.2017

Ndugulile alisema kwamba takwimu za Shirika la Afya zinaonesha kwamba jumla ya watu mil 253 wana matatizo ya kuona na wengi wao wanatoka kwenye nchi zilizoendelea na maskini ikiwemo Tanzania.

Aidha takwimu zinaonesha kwamba ifikapo 2030 vifo vitokanavyo na kisukari vitaongezeka maradufu ulimwenguni kote,takwimu pia zinaonesha Shinikizo la damu linaongoza bara la Afrika kwa asilimia 46 ikilinganishwa na asilimia 35 katika bara la America lenye idadi chache katika Shinikizo la damu.

Hata hivyo inakadiriwa takribani asilimia 1 ya watanzania wana ulemavu wa kutoona na asilimia 4 wana upungufu wa kuona ambapo asilimia 80 ya visababishi vya magonjwa hayo ni vile ambavyo vinaweza kutibika au kuepukika kama vile mtoto wa jicho.

Utafiti uliofanywa na Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani na Taasisi ya NIMRI utafiti ulofanyika 2015 inaonesha viashiria vya magonjwa yasiyo ya kuambukizwa yameonesha kuongezeka na kufanya idadi ya watanzania wenye tatizo la Shinikizo la moyo takribani asilimia 25.9 na kisukari asilimia 9.1.

Ndugulile alisisitiza kwamba kutokana na changamoto ya magonjwa hayo inahitajika juhudi za makusudi kwani magonjwa yasiyoambukizwa ni magonjwa ya muda mrefu na matibabu yake yana gharama kubwa hivyo ni vema kwa pamoja Serikali na Sekta binafsi kufanya kazi ya ziada ya kupambana na janga hili ambalo visababishi vyake vikubwa ni aina ya maisha tunayoishi.

Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Knauf Gypsum Ltd Georgios Zachopoulos alisema huduma hii ya matibabu itakua inafanyika kila mwaka kiwandani hapo kwa lengo la kuisaidia Jamii wenye matatizo hayo.

Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mh Filberto Sanga alitoa shukrani za dhati kwa uongozi wa kiwanda cha Knauf,Lions Club ya Dar es Salaam na Hospitali ya Regency kwa moyo wa uzalendo.

Sanga aliongeza kwamba "tuna viwanda 54 na Sera yetu ni Uchumi wa Viwanda katika muitikio huu ndicho kilichofanyika leo ni matunda ya uwekezaji na Kiwanda cha Knauf walienda mbali zaidi kwa kukutana na uongozi wa Lions Club ya Dar es Salaam kwa lengo la kufadhili matibabu ya Macho, kisukari na Shinikizo la damu kwa siku tatu wananchi wa Mkuranga wamepata fursa pekee kwa kupata matibabu bure.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.