• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Maonyesho ya NaneNane yaleta manufaa kwa wakulima Mkuranga

Posted on: August 10th, 2017



Maonyesho ya sherehe za wakulima na wafugaji Nane Nae kanda ya Mashariki yalifanyika Mkoani Morogoro katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikuhusisha Mikoa ya Pwani, Tanga,Dar es salaam na Morogoro ambapo kwa mwaka huu Maonyesho hayo yaliendana na kauli mbiu isemayo “Zalisha kwa tija mazao na bidhaa za kilimo, mifugo na uvuvi ili kufikia uchumi wa kati”.

Akizungumza wakati wa maonyesho hayo Mkoani Morogoro Bi Rither Barbaydu ambaye ni Mratibu wa Maonyesho ya Nane Nane Wilaya ya Mkuranga alisema maonyesho ya nanenane kwa mwaka 2017 yameleta mafanikio makubwa kwa wakulima na wajasirimali  kwani bidhaa nyingi walizokuja nazo  kwenye maonyesho zilipendwa sana na wananchi waliofika kwenye banda la Mkuranga  walinunua bidhaa mbalimbali kama unga wa muhogo,unga wa viazilishe, korosho, bidhaa za usindikaji na bidhaa za ususi.

Bi Honoratha Mdichei mkulima katika wilaya ya Mkuranga kijiji cha Bigwa ambaye anajishugulisha na kilimo cha pilipili hoho,nyanya,na mbogamboga alisema kupitia maonyesho ya Nanene amejifunza vitu vingi,ikiwemo mnyororo wa thamani wa mazao ya chakula na biashara.”zamani nilikuwa navuna mazao na  yakibaki yanaharibika lakini kwa sasa nimefundishwa namna ya kusindika na hivyo nahifadhi chakula kwa muda mrefu pasipo kuhariba”

Bi Honoratha aliendelea kusema kwamba yeye ni mkulima ambaye anafuata taratibu zote za kilimo ili aweze kupata mazao mengi,ikiwemo kupalilia kwa wakati, kuweka mbolea kwa wakati na kumwagilia maji mengi ya kutosha pale yanapohitajika.

Bi Janeth Mbwambo Meneja wa Mkuranga Cassava Cooperative Joint Enterprises (MKUCACOJE)alisema katika maonyesho ya Nanenane wameleta bidhaa za unga wa muhogo,Unga wa Viazilishe na  bidhaa zinazotokana na muhogo na viazilishe. ”Wateja wengi walipenda na walinunua kwa wingi na wengine walitoa oda na hivyo kusadia kupata masoko  kirahisi kupitia maonyesho ya Nane nane”.Bi Janeth alisema

Aidha bi Janeth aliendelea kusema unga wa viazilishe ulikua kivutio kikubwa kwenye maonyesho hayo kwani wateja waliweza kuona na kuonja bidhaa mbalimbali zilizotengenezwa kupitia viazilishe ikiwemo juisi, uji, keki,maandazi,tambi na kripsi.

Katibu Tawala Wilaya ya Mkuranga Dk.Severine Lalika alisema maonyesho ya Nane nane kwenye banda la Mkuranga yamekuwa hai zaidi ikizingatiwa wakulima waliandaliwa vizuri kwa kutoa maelekezo kuanzia upatikanaji wa mbegu hadi upatikanaji wa bidhaa husika.

Dk Lalika alitoa ushauri kwa maonyesho yajayo jengo liboreshwe vizuri zaidi kwani kwenye maonyesho haya lengo ni kufanya biashara na kutafuta masoko hivyo jengo likiboreshwa wateja wengi watapata hamasa ya kuingia kwenye banda la Mkuranga na hatimaye kuitangaza wilaya ya Mkuranga.

Maonyesho ya sherehe za wakulima na wafugaji Nane Nane kanda ya Mashariki yalifanyika Mkoani Morogoro kuanzia tarehe  01-10/08/2017 yalifunguliwa na Prof.Jumanne Maghembe (MB) Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye alimuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Kassim Majaliwa Majaliwa na kwenye kilele chake yalihitimishwa na Dr.Hamisi Kigwangwala ambaye alimuwakilisha Makamo wa Raisi Mh. Samia Suluhu Hassan.Aidha  Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga imeshika nafasi ya pili katika Mkoa wa Pwani kwenye maonyesho hayo.


Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.