Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

RC Ndikilo apongeza juhudi za kuendeleza utalii, uwekezaji Mkuranga

Posted on: February 27th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo amepongeza juhudi za  Wilaya ya Mkuranga katika sekta ya uwekezaji kwenye Utalii  zinazoendelea kufanyika katika kijiji cha Mpafu kata ya Dondo wilayani Mkuranga.

Ndikilo alisema hayo hapo jana wakati alipotembelea eneo la utalii lililopo kijijini hapo liitwacho Palacha Dream City linalomilikiwa na Zainnudin Adamjee kupitia kampuni ya Global land solution ambao ndio waendelezaji wa  mradi huu ambapo kwa sasa wameshakamilisha mgawanyo wa matumizi ya ardhi ikijumuisha hoteli, nyumba za makazi, masoko, shule, maeneo  ya biashara na huduma za kijamii.

“ kuanzisha jambo hili itakua tumefungua Utalii katika kanda ya kusini “Southern Circuit” kwani utalii kwa kanda hii  bado haujaendelezwa sana lakini  juhudi kama hizi za Global Land Solution zikiendelezwa zitaleta mchango  mkubwa sana kwa jamii na Taifa kwa ujumla.”Ndikilo alisema

Ndikilo alisisitiza kwamba Pwani ina mwambao wa bahari ya hindi kwa takribani kilomita 300 zenye fukwe nzuri, mchanga mzuri, na kwa Palacha Dream city ina kilomita 4  yenye fukwe ndio maana wamepatikana wawekezaji kutoka Dubai na Hispania  ambao watashirikiana na Global land solution kuendeleza Palacha Dream City.

  Mkurugenzi Mtendaji wa Global land Solution bwana  Zainuddin Adamjee alisema “Tutashirikiana na kampuni ya Dubai iitwayo Fahkrudin Properties ambao wamebobea katika ujenzi wa miradi kama hii duniani na kampuni ya Barcelo Group ya nchini uhispania ambao ni mabingwa wa uendeshaji wa hoteli”.

Adamjee aliongeza kwamba kuna changamoto mbalimbali zinazokabili mradi huu ikiwamo Mawasiliano ya simu hafifu, Maji na Umeme kwani unahitajika umeme mwingi kuanzia wakati wa ujenzi wa mradi hadi katika uendeshaji, pia ameomba uboreshaji wa barabara ya Mkuranga kwenda Kisiju ili iweze kuhimili mzigo wa tani 30 na pia barabara ya kutoka Dondo hadi Palacha iunganishwe katika mipango ya barabara hiyo.

Wakijibu changamoto hizo, Meneja wa Tanesco Wilaya ya Mkuranga Mhandisi Regina Mvungi alisema REA awamu ya tatu italeta umeme mpaka kijiji cha mpafu ambapo itakuwa mwezi machi mwaka huu na ndani ya awamu ya tatu kuna hatua tatu, ambapo kwenye hatua  ya pili umeme utafika hadi kwenye eneo la mradi wa utalii Palacha Dream City.

Kuhusu changamoto ya mawasiliano  Meneja wa TTCL kanda ya kusini bwana Ramadhani Mshana alisema kutokana na changamoto hii kampuni yao ina mradi wa uwezeshaji mawasiliano vijijini (UCSAF), lakini kwa sasa wanaweza kutatua changamoto hiyo kwa kutumia satellite broadband ambayo itasaidia kwa kipindi hiki wakati wanaendelea kutafuta suluhu ya jambo hili.

Pia Kuhusu Changamoto ya maji, Meneja DAWASCO kutoka Kibaha bwana Grossman Makere alisema “kwa kuwa tayari walishaanza utaratibu wa kutatua changamoto hii ni vema watupatie andiko la mradi ili tuweze kufanya hatua za haraka”

Mhandisi Peter Shirima Meneja wa TARURA Wilaya ya Mkuranga alisema “Hatukuweka kwenye bajeti ya 2017/2018  na  pia kwenye mapendekezo  ya bajeti ya 2018/2019 ambayo imeshawasilishwa  lakini tutaiandikia  andiko wiki hii na kufanyia upembuzi  ili tupeleke  maombi maalum Wizarani ili tuone kama tunaweza kusaidiwa.

Katika hatua nyingine wakati akitembelea kiwanda cha Lodhia Steel and Plastic Company Limited, Mhe. Mkuu wa Mkoa alieleza kuwa lengo la ziara hiyo ni kutambua Viwanda ambavyo vimekamilika vinavyohitaji kufunguliwa rasmi na viongozi wa juu wa Serikali, ambapo alitaja kuwa viwanda tisa vimekamilika vinavyohitaji ufunguzi huo, viwanda hivyo ni:-
Twyford Ceramic Company Ltd kiwanda cha vigae, KEDS washing Powder kiwanda cha sabuni , Jafra Investment & Suppliers Ltd Mabomba yaPlastiki, Budget Movers Co. Ltd kiwanda cha kuunganisha mabodi yamabasi na Hunan Power Group kiwanda cha Nguzo za zege, Sayona Fruit Processing Plant kiwanda cha kusindika Matunda, na viwanda vitatu vya Lodhia steel anda plastic vinavyozalisha nondo, bomba na plastiki.
Aidha, alitaja faida za kiwanda hicho ni pamoja na kujenga barabara inyoingia kiwandani hapo, ajira zaidi 1500 walizotoa kwa watanzania mchango wao wa mapato kwa serikali.


Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • RO MKURANGA AWAFUNDA WAANDIKISHAJI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI

    May 14, 2025
  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.