• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

RC Ndikilo awajia juu wnaohujumu Mfumo wa Stakabadhi ghalani

Posted on: October 4th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Eng.Evarist Ndikilo amewajia juu baadhi ya vyama ya Msingi  vya Mkoa wa Pwani kwa kuhujumu mfumo wa stakabadhi ghalani kwa kuchanganya mawe na mchanga kwenye korosho .

Ndikilo aliyasema hayo hapo jana kwenye kikao  cha wadau wa Korosho Mkoa wa Pwani kilichofanyika Wilayani Mkuranga kwenye ukumbi wa Kiguza Flex.

Ndikilo alisema”Mkoa wa Pwani umechafuka kwa sababu baadhi ya vyama ya msingi kuchanganya mawe na mchanga kwenye korosho hivyo ni lazima kuwe na maamuzi sahihi kwani huu ni uhujumu uchumi, nchi yetu imechafuka kwa sababu ya watu wachache wanaoharibu ubora wa korosho na uzito kwa lengo la kutengenza fedha ya bure bila jasho,inabidi tutoke huko na tubadilike”

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Eng. Evarist Ndikio akihutubia katika kikao hicho, Kulia ni Mkuu wa wilaya Mhe. Filberto Sanga

Ndikilo aliongeza kwamba mfumo wa stakabadhi ghalani upo ndani ya Ilani ya chama cha Mapinduzi lakini pia ni mfumo ambao umelenga kumkomboa mkulima wa hali ya chini hivyo wale watu wachache wenye lengo la kuhujumu mfumo huu serikali itawachukulia hatua za kisheria.

Ndikilo alisisitiza kwamba magunia ya Mkoa wa Pwani yana alama ya rangi ya kijani hivyo yahifadhiwe kwa uangalifuili yasiangukie kwenye  mikono ya watu wahalifu ambapo yakichukuliwa na watu tofauti yanaweza kuwekewa korosho ambazo sio za Mkoa wa Pwani na kusababisha Mkoa huo kuchafuka.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkuranga Mh Juma Abeid alisisitiza kwamba mfumo wa stakabadhi ghalani upo kisheria na hivyo hauwezi kupingwa na watu wachache na pia serikali haiwezi kupingwa kilichobaki ni utekelezaji tu.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkuranga Mh Juma Abeid akichangia mada katika kikao hicho

Rashidi Selungwi Mdau wa korosho kutoka Wilayani Mkuranga alisisitiza juu ya kuwasimamia viongozi wa vitongoji kwani hutoa takwimu za mikorosho ambayo si sahihi ”Tungekuwa na  takwimu sahihi zingepatikana tani zaidi ya milioni 20 katika Mkoa wa Pwani”

Bei dira iliyopitishwa na Mkutano Mkuu wa wadau wa Korosho kwa mwaka 2018/2019 ni daraja la kwanza Tshs 1550 na daraja la pili ni Tshs 1240.

Maandalizi ya msimu wa korosho 2018/2019 unaendelea vizuri kwani gunia 320,000 zimeagizwa na mzabuni Dirma Holdings Ltd kwa ajili ya kuwekea korosho za Mkoa wa Pwani na magunia hayo yataletwa kabla ya tarehe 09.10.2018.

Aidha matumizi ya Ghala kuu hadi sasa yamepitishwa maghala mawili ambayo ni ghala la Costantine  Mumba-Mwanambaya- Mkuranga na Ghala la TANITA Kibaha.

Wadau wa zao la Korosho kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Pwani wakifuatilia kikao

 Aidha wadau wa Kikao hicho waliomba wapate ghala lingine kutoka Kibiti kutokana na umbali mrefu kutoka Rufiji hadi  Mwanambaya Wilayani Mkuranga kwani pia umbali huo unaweza kusababisha korosho kutoroshwa na kuuzwa maeneo mengine kabla ya kufika eneo husika.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.