• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Serikali yafungia mgodi wa Mchanga Mkuranga

Posted on: September 22nd, 2017

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira Mhe Luhaga Mpina (MB) jana ameufunga mgodi wa mchanga unaomilikiwa na Christopher Lema uliopo katika kijiji cha Kolagwa kata ya Tengelea wakati alipokuwa kwenye ziara yake Wilayani Mkuranga.

Mpina alifikia maamuzi hayo baada ya kuona uharibifu mkubwa wa mazingira ambao umesababisha mmomonyoko  wa ardhi kiasi cha kuhatarisha  maisha ya wapita njia na hasa wanafunzi wanapoelekea shuleni.

Akiongea na wananchi waliojitokeza katika eneo hilo Mpina alisema, “Uchimbaji ulianza kiholela na haukuzingatia taratibu na Taasisi za Serikali yaani Halmashauri,NEMC (Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira) na Wizara ya Nishati na Madini zilikosea ilibidi zijiridhishe dhidi ya uchimbaji wa ardhi na  hatma ya wananchi wanaoishi eneo hilo,inavyoonesha hakuna mkutano wa kata wala kijiji ulioridhia kuhusu uchimbaji wa eneo hili.”

Mh mpina aliagiza ndani ya siku 14 Halmashari ya Wilaya ya Mkuranga, NEMC na Wizara ya Nishati ya Madini wafuatilie athari zilizojitokeza na kuangalia taratibu zote za uchimbaji kama zilifuatwa na ikigundulika taratibu hazikufuatwa  hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya makosa atayopatikana nayo ikiwemo kupigwa faini  kulingana na athari zilizojitokeza au kurejesha mazingira katika hali ya awali.

Katika hatua hiyo pia Mpina alitembelea kiwanda cha Bakhresa na kujionea mazingira ya kiwanda hicho na kupata malalamiko kutoka kwa wananchi wa eneo hilo juu ya kelele kutoka kwenye kiwanda hicho na pia maji ya mvua yanayotiririka na kuingia kwenye makazi ya watu.

Aidha Mpina ameagiza Taasisi za Serikali zinazohusika kupima  kiwango cha sauti au kelele zinazosababishwa  kwenye kiwanda hicho na pia kupima  maji yanayotiririshwa kama yana viwango vilivyoruhusiwa.

Mpina aliongeza kwamba kama majibu yataonesha   kelele zinazidi kwa mujibu wa kanuni za mazingira wataelekezwa kupunguza kelele hizo na maji kama ni machafu hawataruhusiwa na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Mpina alifurahishwa na wananchi wa Mkuranga kwa upendo waliounesha wakati  walipofika kwenye ziara yake na aliahidi kurudi  tena wilayani Mkuranga ili kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo.


Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA 10% KWA MWAKA WA FEDHA 2024-2025

    May 20, 2025
  • RO MKURANGA AWAFUNDA WAANDIKISHAJI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI

    May 14, 2025
  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.