• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

TASAF yabadili maisha ya kaya maskini Mkuranga

Posted on: February 9th, 2018

TASAF awamu ya tatu-Mpango wa kunusuru kaya maskini wilayani Mkuranga ulianza  mwaka 2015 na unahusisha vijiji 77 kati ya 125 na jumla ya kaya 5,045 zilianza kupata ruzuku lakini hadi kufikia sasa kaya 4690 ndizo zinazopokea ruzuku. Kaya 355 zimeondolewa kwa sababu mbalimbali kama kuhama kutoka eneo la utekelezaji au kifo hivyo kukosa sifa za  kuwepo kwenye mpango.

Madhumuni ya TASAF awamu ya tatu ni kuziwezesha kaya kupata mahitaji ya msingi na fursa za kujiongezea kipato na walengwa wa mpango ni kaya maskini katika maeneo yalioainishwa.

Hayo yalisemwa hapo jana  na Mratibu wa TASAF Wilaya ya Mkuranga bwana Kudra Timoth wakati akiratibu  zoezi la uhawilishaji katika kijiji cha Mbulani kata ya  panzuo.

Kwa upande mwingine, Bwana Muharami Makutike Afisa Mtendaji kijiji cha Mbulani alisema mpango wa kunusuru kaya maskini umewasaidia wananchi wa kijijini hapo kwa mafanikio makubwa ikiwemo wengine kujenga nyumba za bati, wakina mama kujiunga kwenye vikundi na kufanya biashara ndogondogo na wengine kufungua migahawa

Alisema, “kwenye kijiji changu nina walengwa 115 na kati ya hao walengwa 28 wanalipwa kwa njia ya mtandao  na walengwa 87 wanalipwa kwa njia ya fedha taslimu. Hali zao za maisha sasa zinaridhisha tofauti na ilivyokuwa awali; naipongeza serikali”

Bi Halima Ally mkazi wa kijiji cha matanzi kata ya Beta alisema “Naishukuru sana Serikali kwa kunisaidia kuingia kwenye mpango huu wa kunusuru kaya maskini kwani nilikuwa napata tabu mimi na familia yangu kwa kuishi kwenye nyumba ya makuti lakini kwa sasa nalala kwenye nyumba yenye bati.”

Mwenyekiti wa kijiji cha Matanzi bwana Ibrahim Mkenda anasema changamoto kubwa anayokutana nayo kwenye mpango huu ni baadhi ya wananchi kuonekana kuwa na makazi duni na kuingizwa kwenye mpango huu ingawa wana uwezo wa kupata fedha,vilevile kuachwa kwa baadhi wa wananchi wasiojiweza sababu ya kuwa ndugu zao wana uwezo wa kuwahudumia.

TASAF awamu ya tatu-Mpango wa kunusuru kaya maskini unawezesha kaya maskini umewezesha kaya maskini kupata mahitaji ya msingi, kulinda rasilimali zao na kuweka akiba kwa ajili ya kujiletea maendeleo na hatimae kijitoa kwenye umaskini.

Vilevile Mpango huu umesaidia kuleta mafanikio kwa walengwa na jamii kwa kupunguza vifo vya watoto na wazee na kupunguza utoro kwa watoto hawa walio katika kaya maskini. Pia walengwa wengi wamejiunga katika vikundi vya uzalishaji maji na kumekuwa na ongezeko la wanafunzi wanaohudhuria shuleni na kwenye vituo vya afya


Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.