• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

TASAF yanufaisha vijiji 77 wilayani Mkuranga

Posted on: February 23rd, 2018

MFUKO wa Maendeleo ya Jamii,Tasaf, umeziwezesha familia zilizokuwa na
kipato cha chini na makazi duni, kuzipatia kipato ambapo wameweza
kunufaika kimaisha kutokana na jamii kuwa na kipato duni na makazi duni hali hiyo
ilisababisha hata kushindwa kula milo mitatu na wengine kushindwa hata
kuwapeleka watoto shule kutokana na kukosa fedha za kujikimu na
kununua chakula cha milo mitatu.
Katika kukabilina na changamoto hizo, Mkuranga ni miongoni mwa Wilaya
ambazo wakazi wake wamenufaika na ruzuku kutoka Tasaf na hali hiyo
imewasaidia kuboresha makazi yao ikiwamo  kula milo mitatu,kuwapeleka watoto shule ,kupata ajira na kuwapeleka watoto kliniki.
Hayo ni maneno ya mmoja wa wanufaika wa Tasaf anaelezea hali ya maisha
yake kwa sasa.
Halima Ally anasema yeye alikuwa akilala katika chumba kimoja
kilichoezekwa na majani na akiwa na watoto nane.
Anasema yeye ni mkazi wa kijiji cha Matanzi Kata ya Beta Wilaya ya
Mkuranga Mkoani Pwani, anasema chumba hicho ndicho alichokuwa akiishi
na watoto wake nane na humohumo ndipo alipokuwa akipikia.
Anasema aliingizwa katika tasaf mwaka 2015 na amekuwa akilipwa kiasi
cha shilingi elfu 60 kila baada ya miezi miwili.
“Nilianza kulipwa fedha hizo sikuchezea maisha nilikuwa nanunua
mabati naweka na mpaka nilipoweza kujenga nyumba na kuiweka
mabati,’’anasema.
Anasema katika maisha yake amefanikiwa kupata watoto nane ni wawili
ambao wanasoma shule na wengine hawakuweza kuingia shule kutokana na
kushindwa kuwasomesha kwa kutokuwa na kipato.
Anasema kazi yake kubwa ni kuwalimia watu mabondeni ili aweze kumudu
maisha, lakini pamoja na kilimo hicho cha kuwalimia watu hakuweza
kubadilisha maisha yake kama ilivyo kwa sasa baada ya kuingizwa
Tasaf.
Anaongeza kuwa anaishukutu sana Tasaf ambayo imeona hali ya maisha
yake na kuyabadilisha na kumfanya leo analala katika nyumba iliyobora
na salama.

Juma Rashid ambaye ni mume wa Halima anasema kuwa, anaishukuru TASAF
kwa kuwaboreshea maisha yao.
Anasema awali walikuwa wakiishi katika chumba kimoja cha majani,
lakini leo hali yao ya maisha imebadilika na kuishi katika nyumba
iliyokuwa ya kisasa.

Afisa Mtendaji kata ya Beta, Ally Nassoro Mbalika anasema kuwa,
mpango wa TASAF katika kata hiyo umeingia mwaka 2015.
Anasema walengwa wamenufaika na fedha hizo, ambapo wapo walio nunua
mifuko, mabati na kutengeneza nyumba zao.
Anasema katika mafanikio hapakosi changamoto na kuongeza kuwa, kuna
baadhi ya watu ambao hawakuwapo katika mpango huo wa ruzuku, lakini
baada ya kukimbilia mjini na waliposikia watu wananufaika, wakarudi
vijijini na kutaka waingizwe katika mpango huo.
Anasema kuna utaratibu wa watu kupata fedha za ruzuku na sio kila mtu
ambaye anaingia kijiji anapata fedha bila ya kupitia taratibu na wale
wasiojua hilo, wanatoa malalamiko kuwa wameachwa kuingizwa katika
mpango huo.
Asha Kondo anasema TASAF imemsaidia kuboresha nyumba yake, kwa kuweka
mabati na kuongeza kuwa anapata kila miezi miwili elfu 44.
Mtendaji kijiji cha Mbulani Muharami Mwakitika anasema walengwa
katika kijiji chake wapo wanaorushiwa kwa njia ya mitandao na wapo
wanaopewa kwa njia ya kawaida.
Anasema katika kijiji hicho kuna watu ambao wamelipwa kiasi cha
shilingi milioni 6.7 kwa njia ya kawaida na kiasi cha shilingi milioni
10 kimelipwa kwa watu wa njia ya mtandao.
Anasema palipo na mafanikio napo hapakosi changamoto ambapo kuna
baadhi ya watu wamepoteza laini za simu na hali hiyo imekuwa
ikiwafanya wawapatie maelekezo ili kwenda kwa mawakala wapatiwe laini
zingine.
Anasema kuwa kuna baadhi ya walengwa ambao ni wazee wanaishi vijijini,
wanaingiziwa pesa, lakini kutokana na mtandao kusumbua wamekuwa
wakilalamikia kutopata pesa.
Anasema walengwa walionufaika na ruzuku, wameweza kununua mbegu na
kulima, wapo walianzisha migahawa,wapo walioboresha migahawa yao na
wapo walioboresha maisha .
Asma Magoma anasema TASAF  imemwezesha kufuga kuku kwa kupatiwa elfu 44
pia watoto wanahudhuria masomo na kuongeza kuwa kibanda chake
kilichokuwa kinavuja sasa kakiwekea mabati.



Zakia Said Mkonge anasema yeye kafungua mgahawa kutokana na kupata
fedha kutoka TASAF.
Anasema awali alikuwa akipokea elfu 48,000 sasa anapokea elfu 42.
Kwa mujibu wa Mratibu wa TASAF Mkuranga  bwana Timoth Kudra anasema kuwa,
zaidi ya shilingi bilioni mbili, zimetolewa kusaidia kaya masikini
kuboresha mfumo wa maisha.
Anasema hayo alipotembele katika vijiji mbalimbali na kuziona familia
ikiwamo na wengine kuchukuwa ruzuku.
“Wilaya ya Mkuranga ina vijiji 125, vijiji 77 vipo katika mpango wa
TASAF ambapo mpaka sasa kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni mbili,
kimetolewa kwa walengwa wanaonufaika na mfuko huo,’’anasema

 kuwa mwaka 2014 walianza kwa kuibua kaya masikini, ambapo mwaka
2015 walianza na utekelezaji.
Anasema kaya 4,690 zimenufaika na ruzuku hiyo.
Anasema kuwa, Katika Wilaya ya Mkuranga, wanawalipa kaya masikini,
ruzuku ya msingi, na masharti.
Anasema katika ulipaji zaidi ya watu 3000 wanalipwa kwa njia ya
kawaida na zaidi ya watu 1900 wanalipwa kwa njia ya mtandao.
Anasema huo ni mzunguko wa 16, lakini katika ulipaji wa njia ya
mtandao kumekuwapo na changamoto ambapo baadhi ya watu kutokuwa na
vitambulisho vya kupigia kura na wengine kutojua kusoma na kuandika.

Anasema ruzuku imeboresha malengo ya walengwa.
Anasema kaya zilizokuwa zikipata mlo mmoja nazo ziliingia katika
vigezo vya kupata fedha.
Anaongeza kuwa utimizaji wa masharti unatakiwa kuzingatiwa Anasema
kama wazazi au walezi wasipopeleka watoto shule hao wakikuta kuna
changamoto katika malipo wanalalamika.
Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.