• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Ulega akutana na Wazee wa Kisiju

Posted on: November 27th, 2019

Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Mkoa wa Pwani ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi  Abdallah Ulega  amefanya ziara katika Kata ya Kisiju kwa kutembelea bandari ndogo ya Kisiju kujionea changamoto katika bandari hiyo pamoja na kukutana na Wazee wa  Kisiju ambao wamemtuma awafikishie kilio chao kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Wakimsomea muhtasari wa Kikao maalumu cha wazee kilichowajumuisha Madiwani wa  Kata ya Dondo na Kisiju kwenye ukumbi wa Shule ya sekondari Sotele juzi, wazee hao maarufu wamemwomba Rais wao ambaye ni msikivu na mtetezi kwa wanyonge ahakikishe anawaletea Barabara ya Lami kutoka Mkuranga hadi Kisiju Pwani kabla mauti hayajawakuta.

Wakiendelea kuwasilisha taarifa hiyo  kwa Kiongozi huyo kwenda kwa Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa (CCM) Taifa, wazee hao wanaomba kushushiwa  umeme katika baadhi ya Vijiji kwani pamoja na kutoa maeneo yao yakiwemo mazao lakini baadhi ya Vijiji vyao nishati hiyo tegemeo katika kuanzisha Miradi mbalimbali imewaruka na kubaki gizani.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa (CCM) Wilaya ya Mkuranga Mzee Ally Msikamo aliungana na wazee wenzake kumsisitiza Mbunge wao awafikishie ujumbe huo kwa Rais kama ulivyo hatmaye kilio chao kipate ufumbuzi kwani wanasema tangu wazaliwe hadi umri unaelekea kuwaacha suala la kuwepo kwa barabara ya lami wanasikia kwa wenziwao tuu huku wakiweka bayana umuhimu wa Barabara hiyo kwamba ni muhimu kwa kuwa  inapitisha korosho zaidi ya tani elfu kumi kila mwaka sambamba na fursa ya uwekezaji kwenye fukwe mbalimbali.

Naye Mbunge Ulega baada ya kupokea Muhtasari huo aliwahakikishia kuwa mambo yote atayafanyia kazi sambamba na kuwasilisha maombi yao hayo kwa  Rais, lakini pia amewaambia wazee hao kuwa suala la bandari atalisimamia kwa kadri ya uwezo wake ili isife kwani anajua umuhimu wa Bandari hiyo kwa wananchi wa Kisiju na Halmashauri kiujumla.

Aidha aliwataka wananchi wote ambao hawajalipwa fedha zao za Korosho kuandika majina yao na taarifa zao aweze kuwasaidia  ili kila mmoja awe kukamilisha mipango yake ukizingati tayari msimu mpya wa zao hilo umeanza.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.