• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mkuranga wakabiliwa na tatizo la utapiamlo

Posted on: August 18th, 2017


Wilaya ya Mkuranga iliyopo katika Mkoa wa pwani inakabiliwa na tatizo la ugonjwa wa utapiamlo kutokana na kuwepo kwa lishe duni kwa baadhi ya wakazi wa Wilaya hiyo.

Mbali na lishe duni,pia imebainika kuwa ugonjwa  wa UKIMWI umechangia kuwapo na ugonjwa huo kutokana na kuwapo wategemezi wengi katika familia.

Kuzalisha chakula kisichotosheleza mahitaji ya mwaka,hali duni ya uchumi ya jamii kutokana na kuwa na kipato kidogo.

Makundi ambayo yameathirika na utapiamlo katika wilaya ya Mkuranga ni kina mama wajawazito, na watoto wenye umri chini ya miaka mitano ambao ukuaji wao ni wa shida.

Kaimu Mratibu wa Lishe Wilaya ya Mkuranga Bi Shani Tonga akiongea na Afisa Habari Mkuranga bi Boppe David wakati wa mahojiano katika ofisi ya Afya Wilaya alisema wagonjwa wa utapiamlo wilayani wanapatiwa tiba na lishe ya bure kwa wagonjwa wenye utapiamlo mkali.

“ushauri wa lishe unatolewa kwa wazazi, walezi na kwamba ushauri unahusisha unyonyeshaji wa mama kwa miezi sita.” Alisema

Anaongeza kuwa ulishaji  wa watoto kuanzia miezi sita hadi 59 (miaka mitano kasoro mwezi mmoja) unaendana na kuwepo elimu ya lishe kwa wagonjwa hasa katika hospitali ya wilaya ya Mkuranga.

Miongoni mwa mambo yanayofuatiliwa ni kuchunguza hali ya lishe kwa wagonjwa waliopo na ushauri katika masuala ya ulaji kwa motto aliye na umri chini ya miezi sita.

Bi Shani alisema kuwa jamii bado ina uelewa mdogo kuhusu maandalizi na ulaji katika jamii.kuongezeka kwa kasi ya ugonjwa wa UKIMWI inasababisha kuwapo wategemezi wengi katika familia na inapunguza uwepo wa akiba ya kutosha ya chakula kwani wazalishaji wanakuwa wamepungua.

Anaongeza kwamba Mkuranga ni miongoni mwa Wilaya zenye tatizo la utapiamlo, viashiria vyake  vikiwa upungufu wa damu na waathirika wakubwa ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano, wajawazito na wanawake walio katika umri wa kuzaa.

Wengine ni wagonjwa wa muda mrefu, yatima, wazee na watoto waishio katika mazingira  magumu.

Akizungumzia katika kipindi cha 2015 kuhusiana na utapiamo Shani alisema wagonjwa hospitalini kutokana na maradhi hayo walikuwa 3701 na kati yao 290 sawa na asilimia 7.8 walikuwa na viashiria vya upungufu wa damu.

Anaongeza kuwa kwa waliopata elimu ya lishe na unyonyeshaji walikuwa 1412 ni sawa na asilimia 39.1 na waliopewa rufani wako 319 ambao ni sawa na asilimia 8.9.

Mkurugezi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga mhandisi Mshamu Munde alisema kuwa mkakati wa  wilaya  ni kuendelea kutoa elimu ya lishe kwa jamii ili kumaliza tatizo la upungufu wa damu katika wilaya ya Mkuranga.

Munde anaendelea kusema  kwamba Halmashauri itaendelea kutenga bajeti ili kukidhi masuala ya lishe wilayani ikiwemo kuwa na walimu wa afya na wanafunzi watahusishwa kwa kuhamasishwa ulimaji wa bustani za mbogmboga na viazilishe.


Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA 10% KWA MWAKA WA FEDHA 2024-2025

    May 20, 2025
  • RO MKURANGA AWAFUNDA WAANDIKISHAJI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI

    May 14, 2025
  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.