• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jukwaa la Wanawake lazinduliwa Mkuranga

Posted on: June 30th, 2017


Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Filberto Sanga amezindua rasmi jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi wilayani Mkuranga hapo jana ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mheshimiwa Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama samia Suluhu Hassan kuwa kila Wilaya iunde jukwaa la wanawake.

MKuu wa Wilaya huyo alisema kwamba dhumuni la kuunda jukwaa hili katika wilaya ya Mkuranga ni kuwapa fursa wanawake wa wilaya ya Mkuranga kukutana pamoja na kujadili mambo mbalimbali ya maendeleo yao hasa fursa na changamoto wanazokumbana nazo katika suala zima la maendeleo ya kiuchumi na jinsi ya kushiriki kikamilifu katika biashara na shughuli zingine za kiuchumi, hivyo kupitia jukwaa hili wanawake watapata fursa zilizopo katika wilaya hii ikiwemo viwanda vikubwa na vidogo vinavyozalisha bidhaa mbalimbali ambavyo ni soko la malighafi  na fursa ya ajira.

Aliendelea kusisitiza kwamba jumla ya viwanda 57 vimeanzishwa katika wilaya ya Mkuranga hadi sasa.Vilevile Wilaya ina ardhi yenye rutuba na bora kwa mazao kama mihogo, matunda, korosho ambayo ni fursa  kushiriki katika kilimo cha biashara ili kukuza uchumi wa Mkuranga.

Mkuu wa Wilaya huyo pia ameliagiza jukwaa hili kukutana kila baada ya miezi sita kwa kufanya vikao vyake na kuwasilisha taarifa za vikao katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji pamoja na ofisi yake ili kujua kitu gani kinaendelea katika jukwaa hilo, lakini pia aliwaagiza waratibu wa uwezeshaji ngazi ya kata kuhakikisha wanaunda majukwaa ya uwezeshaji wanawake kiuchumi katika kata na kuwasilisha taarifa hizo kabla ya Novemba 30 2017.

Mwenyekiti wa Jukwaa hilo bi Mariama Ulega aliwashukuru wakina mama wa Mkuranga kwa kumchagua kuwa Mwenyekiti wa Jukwaa hilo na  aliahidi kufanya kazi kwa uwezo wake wote bila kujali itikadi ya chama, dini wala kabila na kuhakikisa wanawake wa Mkuranga wanasonga mbele.

Mratibu wa Jukwaa hili Bi Sylvia Gordon ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii alitoa rai kwa Taasisi za kifedha na mashirika mbalimbali kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kwa wakati pamoja na huduma stahiki bila vikwazo na urasimu wowote ili kuwarahisishia kujukwamua kiuchumi.

Wanawake wamekuwa hawapati fursa za kutosha za kiuchumi hapa Tanzania na duniani kote,Hivyo Taifa limeona kuwa ushiriki wa wanawake katika shughuli za uchumi ni kichocheo kikubwa cha maendeleo ya nchi yetu na jamii kwa ujumla kwa sababu ushiriki wa mwanamke katika uchumi unalete mabadiliko makubwa sana katika uchumi wa familia na jamii kwa ujumla.

Katika harakati za kufikia malengo endelevu ya 50/50 ifikapo 2030 ambayo pia yanasisitiza uwezeshaji wa wanawake kiuchumi katibu wa umoja wa Mataifa aliteua timu ya viongozi na wataalam watakaofanya kazi kama chombo cha kutambua na kuweka mikakati ya kupunguza na kuondoa pengo kubwa ambalo limejengeka duniani sambamba na kuongeza ushiriki wa wanawake katika kukuza uchumi ili kurekebisha hali iliyopo sasa.Katika timu hiyo Mheshimiwa makamu wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mjumbe.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.