• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

VIJIJI 79 VYAPATA UMEME MKURANGA..

Posted on: March 15th, 2022


Vijiji 79 kati ya 125 (Sawa na asilimia 63) vimepatiwa umeme katika mpango wa REA 3 mzunguko wa pili Wilayani Mkuranga.

Katika maelezo ya Mkurugenzi Mkuu wa REA Tanzania Bw. Hassan Saidi leo Machi 15, 2022 wakati akitoa taarifa ya utekelezaji miradi ya Umeme Mbele ya Waziri wa Nishati Mh January Makamba aliyeongozana na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kwa lengo la kutembelea na kukagua miradi ya umeme inayotekelezwa na REA  katika Vijiji vya Mangombe, Mikere na Ngarambe vilivyopo kata ya Njia Nne  Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani.

Bw. Said alisema kuwa vitongoji vilivyopatiwa umeme ni 211 kati ya 476 Sawa na asilimia 44.

Mkuu huyo alifafanua kuwa tayari vitongoji 265 kati ya 476 sawa na asilimia 56 bado havijaunganishiwa umeme na kuwa kati yao vitongoji 44 vitapatiwa umeme katika mradi wa REA3 mzunguko wa pili unaoendelea kutekelezwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Bi. Hadija Nasri Ali aliwasilisha ombi lake  Mbele ya Waziri Makamba na Kamati ya Bunge ya Nishati kuwa kituo cha kufulia umeme kijengwe ndani ya Wilaya hiyo ambayo kwa sasa inao uhitaji mkubwa wa Umeme kutokana na ongezeko la Viwanda.

Wakitoa neno la shukrani mbele ya Waziri Makamba na Kamati ya Bunge, Omari Makumbatu na Ashura Mongo wote wakiwa ni wakazi wa Kijiji cha Mikere wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuwasogezea huduma za umeme karibu na kuwawezesha wazee kupata matibabu nafuu katika vituo vya afya sambamba na upatikanaji wa dawa za uhakika.

Nae Diwani wa kata ya Njia Nne. Ally Mambo ameiomba serikali kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha kuunganisha umeme katika Vijiji vilivyobaki ndani ya kata hiyo.

Kazi ya kusambaza umeme  Vijijini katika Mradi wa REA awamu ya Tatu  mzunguko wa pili katika wilaya ya Mkuranga inatekelezwa na mkandarasi China Railway Construction Electrification Bureau Group (CRCRBG) ambaye kwa sasa anaendelea na usimamishaji wa nguzo na kufunga waya kwenye maeneo mbalimbali Vijijini ambapo hadi sasa tayari mkandarasi amekamilisha ujenzi wa miundo mbinu ya kusambaza umeme katika vijiji saba (7)  ambavyo ni Mponga, Mikere, Mingombe, Mamdimpera, Mamdimkongo Makumbea na Misasa katika wilaya  ya Mkuranga.

Ujenzi katika Vijiji vya Kikundi na Kikoo utakamilishwa ndani ya mwezi machi, 2022 na Mradi huu ni wa miezi 18 na unatarajiwa kukamilika mwezi Disemba 2022

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.