• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Viongozi wa wa Vyama vya Ushirika waaswa kutumia Stakabadhi Ghalani

Posted on: October 19th, 2018


Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Bwana Peter Nambunga amewataka viongozi wa  vyama vya ushirika Wilaya ya Mkuranga Kufuata mfumo wa stakabadhi ghalani katika mafunzo yaliyofanyika leo kwa viongozi hao katika Wilaya ya Mkuranga.

Nambunga alisema kufanyika kwa mafunzo hayo ni sehemu muhimu katika kuhakikisha wako tayari kuingia katika utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani”Ifahamike kuwa viongozi wa vyama vya ushirika wanalo jukumu kubwa katika kuhakikisha kuwa mnamkomboa mwanachama na mkulima ambaye si mwanachama kwa kukusanya korosho zilizo bora ambazo zitakuwa zimedarajishwa kutoka kwa mkulima ili zipelekwe kwenye ghala la mnada tayari kwa kungojea wanunuzi wanunue korosho zetu”alisema Nambunga

Nambunga aliongeza kwamba mafunzo hayo yatawasaidia kujua muongozo namba moja wa Bodi ya korosho ambayo inajumuisha majukumu ya viongozi wa vyama vya ushirika katika utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani na kupitia mikataba yenye tija kwa watendaji wa vyama vya ushirika.

“Natambua kuwa kuna baadhi ya vyama havijakamilisha taratibu za kisheria,baadhi yenu mmeshindwa hata kurudisha mrejesho kwa wanachama wenu kutokana na shughuli mlizosimamia msimu uliopita”Nambunga alisema.

Afisa Ushirika Wilaya bwana Valentine Shija alisema “Msimu wa 2017/2018 vyama vya ushirika 44 vilifanya kazi ya kukusanya korosho za wakulima,kati ya hivyo 26 tu ndio vilikamilisha taratibu za kisheria ili viweze kufanya kazi msimu wa 2018/2019”.

Shija aliongeza kwamba vyama vilivyobaki vilikuwa na baadhi ya changamoto ikiwemo kutokuwa na uongozi au idadi pungufu iliyotokana na kujiuzulu baadhi ya vongozi na wengine kusimamishwa,kutokuwa na watendaji wenye sifa au baadhi ya wajumbe wa bodi kufanya kazi za makatibu jambo ambalo limepelekea kuwepo na migogoro au kutokamilisha majukumu ya chama kwa ufanisi.

Shija alisisitiza kwamba “Mikakati ya kutatua changamoto hizi inaendelea kupitia usimamizi wa mara kwa mara,kaguzi za ndani na nje na kuvipa muda vyama ambavyo havina vigezo kujiandaa ili msimu wa 2019/2020 viwe vimekamilika kufanya kazi za chama”.

Mrajisi Mkoa wa Pwani  Angela Nalimi alisema hapo awali kulikuwa hakuna mfumo rasmi wa uuzaji wa korosho  lakini serikali ikaona itafute  chombo imara ambacho kitasimamia wakulima na chombo kilichoonekana  kinafaa ni chama cha ushirika. “Tukapewa dhamana ya kukusanya korosho ya wakulima pamoja na wanachama wetu  kuiuza kwa mfumo wa stkabadhi ghalani sasa kwakua tumepewa jukumu na Bodi ya korosho imetoa mwongozo tukaona sisi kama wadau muhimu tuusome huo muongozo tuuelewe na tuape ili tuweze kutekeleza”Nalimi alisema”

Husna Mbata kiongozi wa chama cha ushirika Kilimahewa alisema”Tumeongea na wanachama wetu ambao pia ni wakulima na tumeongea nao kuhusu  mfumo wa stakabadhi ghalani kama serikali ilivyoelekeza ili mkulima asiweze kunyonywa tena na tumewaambia wakulima wawe makini katika ukaushaji mzuri wa korosho”

Jumanne Makotwa Kiongozi wa chama cha ushirika kutoka Shungubweni alisema msimu uliopita baadhi ya wakulima walikuwa wakilazimisha kuleta korosho ambazo hazijakauka lakini kwa sasa tutawapa elimu ili walete korosho ambazo zitapata soko.

Makotwa aliongeza kwamba”tutahakikisha tunamwaga korosho zote chini ili kuhakikisha hakuna mchanga wala kokote kwenye magunia ya korosho”

Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga ina jumla vya vyama vya ushirika 48 ambavyo vinapatiwa mafunzo kwa lengo la kutekeleza majukumu yao pasipo kuvunja sheria katika uuzaji wa korosho kwa kutumia mfumo uliokubalika na Serikali ambao ni stakabadhi ghalani.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.