• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

vyama vya msingi vyapewa mafunzo Mkuranga

Posted on: November 14th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani Philiberto Sanga amewataka viongozi wa Vyama vya Msingi ( AMCOC )  kuzingatia miongozo ya utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi Gharani ili kuepukana na sintofahamu kwa wakulima wa zao la Korosho kama ilivyotokea katika msimu uliopita.

Akifungua mafunzo kwa vyama hivyo leo katika ukumbi wa Parapanda Mkuranga Sanga aliwataka washiriki kuwa makini na mafunzo hayo na kuwataka kuyafanyia kazi na  hatimaye uwe mwarobaini wa kumaliza  changamoto mbambali kwa wakulima wa zao la Korosho.

Sanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye aliwakilishwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Mhandisi Mshamu Munde alitumia fursa hiyo kuwaonya viongozi hao kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atayekwamisha malipo ya korosho kwa wakulima katika msimu huu.

Pamoja na hayo alisisitiza zaidi kwa kuwageukia walanguzi wa korosho “Kangomba” kwamba watafute kazi nyingine ya kufanya ili kuepukana na mkono wa sheria kama ambavyo Rais Dkt John Pombe Magufuri ameagiza.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri  Julita Bulali pamoja na kuipongeza Benki ya NMB Tawi la Mkuranga kwa kudhamini mafunzo hayo aliwataka viongozi hao wahakikishe mfumo unawanufaisha wakulima , Halmashauri na Serikali kwa ujumla.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Juma Abeid akifunga mafunzo hayo, aliwataka viongozi wa vyama hivyo kutenda haki kwa wakulima huku akiwaagiza makatibu wasifanye kazi kwa mazoea ili kuepuka taasisi ya kupambana na kuzuia rushwa ( TAKUKURU ) Mkuranga, kuwachukulia hatua kwani wao watazingatia sheria , taratibu na kanuni, pia amemshauri Mrajisi Msaidizi Mkoa wa Pwani ikiwezekana kuwaondoa Makatibu wote  waliovuruga msimu uliopita na waajiriwe makatibu wengine wenye sifa.

Mafunzo haya yanafanyika ikiwa ni mkakati wa kulifanya zao hilo la Korosho  linakuwa na thamani kubwa na hasa ukilinganisha na umuhimu wake kwani ni miongoni mwa mazao ya kimkakati nchini.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.