• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Wabadhilifu wa zao la Korosho kuchukuliwa hatua

Posted on: October 30th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Evarist Ndikilo ameziagiza Kamati zote za Ulinzi na Usalama za Wilaya Mkoani Pwani kuwachukulia hatua watu wote watakaogundulika kufanya ubadhilifu kwa wakulima wa Korosho na kuzitaka kamati hizo kumpa taarifa za utekelezaji huo ndani ya siku saba.

Akifungua  Mkutano wa wadau wa Korosho Mkoa wa Pwani uliofanyika katika ukumbi wa Flex Garden Kiguza Wilaya ya Mkuranga Ndikilo amezitaka taasisi zote za fedha zilizoshiriki katika kufanya malipo kwa wakulima wa Korosho kutoa ushirikiano wa kutosha kwa vyombo vya Ulinzi na Usalama za Wilaya ili kubaini kasoro zilizosababisha baadhi ya wakulima kutopata fedha zao

Aidha amempongeza Rais John Pombe Magufuli kwa kufanya maamuzi ya busara kwa kununua korosho zote msimu wa 2018/2019 na kusema hadi sasa Serikali imeshafanya malipo kwa wakulima wa Korosho kiasi cha shilingi Bilion 47.7 na kubaki kiasi cha shilingi bilioni 18.1 ambazo wakulima hawajalipwa.

Ndikilo amewahakikishia wakulima wa zao hilo Mkoa wa Pwani kuwa Korosho zote zilizokusanywa na Serikali zimeshauzwa na kuwataka wawe na subila ili kuona Serikali inamalizia kuhakiki mapungufu yaliyopo ili kila mkulima aweze kupata fedha zake.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga akijibu swali kwa wadau wa Mkutano huo wa Korosho amesisitiza kwa upande wa Wilaya ya Mkuranga hatovifumbia macho Vyama vya Msingi au viongozi wa Vyama hivyo na kuahidi kuwachukulia hatua kali wale wote walioshiriki kufanya ubadhilifu sambamba na kurudisha fedha na hata kuvifuta baadhi ya vyama vya Msingi ambavyo vitaonekana havina tija kwa wakulima wa Korosho Wilayani humo.

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho (CBT) Francis Alfred amesema wao kama bodi ya korosho wanaahidi kutoa mafunzo kila kijiji ndani ya Mkoa wa Pwani katika zao la Korosho ili kuifanya korosho ya Pwani inakuwa na ubora kama ilivyo mikoa mingine.

Chama kikuu cha ushirika mkoa wa pwani (CORECU) kimetakiwa kuandaa magunia mapema sambamba na maghala ili kujiandaa na msimu wa mwaka 2019 – 2020 huku wakulima wakitakiwa kutochanganya Korosho na michanga au takataka zozote kwa lengo la kuongeza uzito.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.