• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Wajasiriamali Mkuranga wapewa mtaji wa kuku

Posted on: August 16th, 2018


Wajasiriamali wilayani Mkuranga wamepatiwa Kuku zaidi ya 1000, kama mtaji ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuondokona na umaskini.
Akipokea Kuku hao hapo jana kutoka kwa kampuni ya AKM greeter iliyoahidi kutoa Kuku 4000,Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mh Filberto Sangaamewataka wakina mama wote watakao nufaika na Kuku hao wasitumie kwa kitoweo bali wafuge ili waweze kuinua vipato vyao vya familia zao.
Aidha Sanga amesema kuwa matarajio yao baada ya mwaka mmoja wakina mama hao hawatakuwa na hali walizonazo sasa."watanufaika katika mambo mengi sana,moja wapo watapata mayai ambayo watauza na Kuku wakizaliana watauza na kuongeza kipato cha familia"alisema 
Sanga aliongeza kwamba kina mama wa Mkuranga wanabahati sana kuliko wenzao kwa hiyo watumie nafasi hiyo kwa ajili ya kujinufaisha."Mbunge ulega anafanya kazi nzuri sana na nampongeza,kina mama msimwangushe"alisema sanga
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mkuranga Mhandisi Mshamu Munde amesema jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi wilayani Mkuranga liliendesha mafunzo ya siku mbili kwa wajasiriamali walijifunza,jinsi ya kutunza fedha na kufanya biashara kwa tija,ambapo katika mafunzo hayo wajasiriamali hao waliahidiwa kupewa Kuku 4000 ili wafuge kwa ajili ya kujikimu kiuchumi na kuondokana na umaskini,ambapo kwa awamu ya kwanza wamekuja Kuku 1058 waliogaiwa kwa wajasiriamali 100 kwa kila mmoja Kuku kumi.
Aidha Munde amewataka kinamama hao kwenda kutumia utaalam waliopewa kwenda kutoa elimu kwa wengine na kuleta tija kwa taifa kwa kujiongezea kipato chao na familia
"Kwenye mafunzo waliambiwa Kuku waliopewa sio zawadi,kuku wale wamepewa ili waweze kuwafuga na kuzalisha kwa hiyo maana yake wamepewa Kuku kumi lakini baada ya muda watatakiwa wawe na Kuku zaidi."alisema Munde
Munde alisisitiza kwamba wana imani sana na wale wote waliopata Kuku watawaendeleza na kuleta matokeo chanya.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa jukwa la kuwezesha wanawake kiuchumi Wilayani Mkuranga bi Mariamu ulega aliwashauri wakina mama wa Mkuranga kutumia Kuku hao kama chachu ya maendeleo ili kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ya hapa kazi tu na kuifanya Tanzania ya viwanda."kina mama tuamke kama Mh.Rais anavyosema tulete Tanzania mpya,tutoke majumbani hakuna kitu kitakacho tukomboa zaidi ya kufanya kazi. "Alisema Mariamu
Kwa upande mmoja wa wajasiriamali waliokabidhiwa Kuku hao bi. Sauda Pazi alisema wanamshukuru Mbunge wa Jimbo
La Mkuranga Mh Abdalah ulega, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo,Mkuu wa Wilaya pamoja na Mwenyekiti wa jukwaa la wanawake kwa msaada huo,ambao alisema watautumia vizuri katika kujikwamua kiuchumi.


Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.