Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

WANAFUNZI 20 KURUDI SHULE

Posted on: March 7th, 2022

Wanafunzi 20 waliokatishwa masomo yao kwa kupata ujauzito kwa bahati mbaya wamerudi shule kuendelea na masomo yao wilayani Mkuranga mkoani Pwani baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuagiza wanafunzi hao warudi shule kuendelea na masomo yao.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Khadija Nassir Ally katika maadhimisho ya siku ya mwanamke kiwilaya katika viwanja vya shule ya msingi Mkuranga

Amesema kwa taarifa alizonazo wasichana hao 20 walikwishajifungua   waliomaliza kunyonyesha watoto wao sasa wamerejea shuleni.

Khadija alisema hiyo sio taarifa nzuri lakini ni taarifa nzuri, ni taarifa nzuri kwasababu pale walipoona giza kuendelea na ndoto zao lakini sasa wanaendelea na ndoto zao kwa kurekebisha makosa yao waliyofanya.

"Ni taarifa nzuri kwasababu unapojikwaa na kuanguka unapoinuka hautainuka na mguu ule ule uliojikwaa yaani wadogo zetu waliojikwaa na kupata ujauzito sasa wataenda kufanya vizuri na kuwa mfano kwa wengine" alisema Khadija.

Aidha aliwataka Walimu kuwasaidia wasichana waliopata changamoto za namna hiyo kwasababu kikawaida kisaikolojia wasichana hao hawawezi kuwa sawa na wasichana wengine.

"Na ndio maana tumewawekea utaratibu wa kupata elimu ya watu wazima na tusiwaache kwasababu wazazi wao peke yao hawataweza kusimamia maendeleo ya wasichana hao bila sisi serikali, Walimu pamoja na Walezi kushirikiana kwa pamoja" alisema.

Hatahivyo Mkuu huyo wa Wilaya ya Mkuranga alionesha kukerwa na baadhi ya wazazi ambao watoto wao wamefaulu darasa la saba lakini hadi sasa bado hawajaripoti shuleni kuendelea na masomo yao na sekondari.

Khadija alisema serikali imefanya jitihada kubwa kujenga madarasa na kuhimalisha miundombinu ya elimu wilayani humo kwa gharama kubwa kubaki nyumbani na wanafunzi hao ni kutojali na kutothamini jitihada hizo za serikali.

Alisema atawaita wazazi hao kwa kufanya mkutano nao ili kuwasikiliza ili kujua sababu za wanafunzi hao kutoripoti shule na baada ya hapo iwapo bado kutakuwa na wasioripoti tena shuleni hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Meneja wa Bank ya CRDB tawi la Mkuranga Martha Ngowi akizungumzia akaunti mpya ya Malkia kwa wanawake ambayo bank hiyo wameianzisha kwaajili ya kuwasaidia wanawake kuhifadhi fedha zao badala ya kuhifadhi kwenye vibubu majumbani njia ambayo sio salama kwa utunzaji fedha.

Naye Afisa Maendeleo ya jamii wilaya ya Mkuranga Amina Hoja alisema bado jamii kubwa ya wana Mkuranga wanatekeleza mila ya mwanamke kukaa na kusubiri kuletewa kwa mtazamo wa kuwa mume ndiye anapaswa kuhudumia familia peke yake.

Amina alisema uelimishaji unaendelea kufanyika ili kubadili fikra za jamii hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA 10% KWA MWAKA WA FEDHA 2024-2025

    May 20, 2025
  • RO MKURANGA AWAFUNDA WAANDIKISHAJI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI

    May 14, 2025
  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.