• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

wananchi Mkuranga wapanda miti 500,000

Posted on: April 13th, 2018


Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga jana imeadhimisha siku ya upandaji miti kiwilaya ambapo ilifanyika katika kijiji cha mlamleni kata ya Tambani ambapo wananchi wa kijiji hicho wamefanikiwa kupanda jumla ya  miti 1500 ambapo miti mingine imepandwa kwenye shule za sekondari na shule za msingi,chuo cha  ualimu vikindu,watu binafsi, Taasisi,msitu wa hifadhi wa vikindu.

Akizungumza katika zoezi hilo la upandaji miti,Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mh.Filberto Sanga alisema miti ina kazi kubwa kwani inatusaidia kupata nishati ambayo hutegemewa na sehemu kubwa ya watanzania kama vile kuni na mkaa,husaidia kupata malighafi za viwanda vya dawa na mbao,hutunza mazingira,hutunza vyanzo vya maji,majengo na huzuia mmomonyoko wa ardhi.

Mh Sanga  aliongeza kwamba kila mwananchi  lazima ashiriki kupanda miti angalau miti kumi kila mwaka na taasisi kama vile shule zinazotumia kuni kuandaa chakula zinatakiwa kuwa na mashamba ya miti,vijiji na  watu binafsi wanatakiwa kuwa na misitu kwani kwa kufanya hivyo itaboresha hali ya mazingira na kuboresha hali ya hewa kwa kupata mvua kwa wakati muafaka.

Mh Sanga amewaonya wananchi wote wanaofanya shughuli zisizokubalika za kuharibu misitu kama vile kulima, kukata miti na kuchoma mkaa ama kwa makusudi ama kwa kutojali umuhimu wa msitu.

Afisa Mtendaji kata ya Mlamleni bwana Abbas Likonda ameahidi kulitunza eneo lilipandwa miti kwa kushirikina na wananchi wa kijiji hicho.

Aidha bwana Likonda aliongeza kwamba elimu ya utunzaji wa misitau itakuwa ajenga ya kuduma kwa kila mkutano wa kijiji na kata ili wananchi wasiende kinyume na utaratibu waliojiwekea katika utunzaji wa miti.

Mwenyekiti wa vijana kijiji cha Mlamleni bwana Sudi Matimbwa alisema “tunashukuru vijana tumepewa eneo la kufanya mazoezi ambalo lipo jirani na eneo  tulilopanda miti,tunaahidi kila tunapokuja kufanya mazoezi tutakagua miti na baadae kufanya mazoezi ili kuhakikisha miti tuliyoipanda leo hii inakua vizuri”

Maamuzi ya kupanda miti kila mwaka yamefikiwa baada ya kuona misitu katika nchi yetu inazidi kutoweka kutokana na shughuli za kila siku za kibinadamu na hasa matumizi yanayozidi kiwango cha uwezo wa misitu yetu kujizalisha.

Aidha juhudi endelevu zinazofanyika za kurudishia uoto wake asili ni kidogo kulingana na kiwango cha uvunaji,hali hii imesababisha maeneo mengi kukosa miti na kunyemelewa na jangwa,kupata athari za mabadiliko ya tabia ya nchi kama vile mabadiliko ya hali ya hewa, mafuriko, joto kali, mmomonyoko wa udongo,upotevu wa aina nyingi za mimea na kukauka kwa vyanzo vya maji.

Ili kurekebisha na kupambana na athari hizo,taifa limeagiza kila wilaya kupanda miti milioni moja laki tano (1,500,000) kila mwaka katika maeneo mbalimbali hasa katika vyanzo vya maji ambavyo vimekwisha haribiwa na maeneo yaliyowazi bila miti au uoto asili.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.