• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Wananchi Mkuranga watakiwa kupewa elimu ili kupunguza tatizo la lishe duni

Posted on: October 10th, 2018


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Bwana Peter Nambunga amewataka wananchi wa Mkuranga kupunguza tatizo la  lishe duni.

Nambunga aliyasema hayo hapo jana wakati wa kikao cha kawaida cha robo cha kamati ya lishe Wilaya  ambapo alisema ”pamoja na juhudi za Serikali kwa kushirikiana na wadau kuendelea kupambana na lishe duni takwimu zinaonyesha kuwa na upungufu wa damu unaendelea kuwa juu kwa wanawake waliokuwa katika umri wa kuzaa  wapo asilimia 45, watoto chini ya miaka mitano wana upungufu wa damu asilimia 58 wakati uzito pungufu kwa wajawazito ni asilimia 16-30, watoto chini ya miaka mitano uzito wao ni pungufu  zaidi ya asilimia 50 na Utapiamlo mkali ni kuanzia asilimia 5-8 na udumavu ni asilimia 30.

Nambunga aliongeza kwamba Wilaya ya Mkuranga inalima vyakula mbalimbali na vingi inachotakiwa ni wananchi wapewe elimu ya namna ya ulaji wa vyakula hivyo ili kupunguza na kuondoa kabisa tatizo la lishe duni.

Afisa lishe Wilaya Bi. Vumilia Ngandago alisema waathirika wa lishe duni ni makundi yote ya binamu ambapo ni watoto chini ya miaka mitano, vijana, wajawazito,  wanaonyonyesha na wazee.

Ngandago aliongeza kwamba dalili za lishe duni ni upungufu wa damu, ukosefu wa vitamin A ,ukosefu wa madini joto, uzito pungufu, Utapiamlo mkali na udumavu.

Ngandago alibainisha baadhi ya  sababu za lishe duni katika wilaya ya Mkuranga ambapo ni uelewa mdogo wa jamii, kamati na wataalam juu ya ulaji sahihi, kutokuwa na chakula cha kutosha  chenye virutubishi muhimu, kutokuwa na mpango wa chakula mashuleni, mila na desturi ya jamii ya jamii ya Mkuranga, hali duni ya uchumi yaani jamii kubwa ya mkuranga wana  kipato kidogo  chini ya 2000.

“Tumejipanga  kutoa elimu kuanzia ngazi ya wilaya, kata mpaka vijiji kwani tukiwaelimisha na wao watasaidia kuelimisha kwenye vikao mbalimbali katika maeneo yao kuhusu lishe na hivyo kupunguza unasihi wa lishe.”Ngandago alisema

Mhe. Hassan Dunda Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Afya na Maji na Diwani wa kata ya Mkamba alisisitiza kwa kusema kwamba wataalam wahusike kuwasaidia wananchi kuhusu suala la lishe kwa kutoa elimu kuanzia ngazi za vijiji hadi kata kwa kutumia maonesho ya sinema ambazo zinaonyesha athari za lishe duni na namna ya kula vyakula bora ambavyo vitaondoa tatizo hilo.

Faviana Mlaki mdau wa lishe kutoka asasi ya Jipeni Moyo Women Community Organization(JIMOWACO) alisema” asasi yetu itasaidiana na Halmashauri ili kutekeleza suala la lishe vizuri  kwakua tunatekeleza mradi kupitia watoa ushauri katika ngazi za  vijiji na kaya hivyo tutawaelimisha kuhusu lishe na wao wataenda kwenye kila kaya kutoa elimu hiyo ili kuondoa kabisa tatizo la lishe duni katika wilaya yetu.”

Kikao hicho kiliibuka na mikakati mbalimbali ya namna ya kuepuka na kuondokana na hali duni ya lishe kwa kuendelea kutoa tiba, kuelimisha jamii kuhusu masuala ya lishe kwenye sekta mbalimbali, kuendelea kuomba wadau waliopo wasaidie kuhamamisha na kutoa elimu, kuimarisha mfumo wa ukusanyaji wa taarifa sawasawa na viashiria vilivyopangwa na kamati ya lishe wilaya kila mmoja kwa nafasi yake awajibike kutoa elimu, na kutoa elimu kupitia redio, sinema, vipeperushi na majarida.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.