• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Wananchi wa Kijiji cha Hoyoyo wachachamaa baada ya shamba lao kuuzwa

Posted on: August 17th, 2018


Wananchi wa kijiji cha Hoyoyo katika kata ya Tengelea Wilayani Mkuranga jana  wakiwa kwenye mkutano Mkuu wa kijiji wamedai shamba lao la kijiji  lenye ekari 12.5 ambalo linadaiwa  limeuzwa kinyume na sheria na bwana Emmanuel Mwakambinga kwenda kwa Celina John Chanja tangu mwaka  2014.

Bwana Mohamed Maluyo Mkazi wa kijiji cha Hoyoyo  anaelezea kwamba shamba hilo walikuwa wanatumia kama shamba la kijiji kwa kilimo tangu mwaka 1984-1985,hivyo kutokana na changamoto  ya upatikanaji wa huduma ya afya wananchi walikubaliana wajenge  zahanati ambapo baada ya kutaka kuanza utaratibu wa kujenga zahanati wakagundua kuna uzio umewekwa kwenye eneo la shamba hilo.

Siti Pazi anasema “kutokana na ukosefu wa huduma ya afya hapa kijiini inatugharimu hasa ukipata uchungu wakina mama tunajifungulia njiani lakini pia usafiri ni wa bodaboda ambao gharama yake kwa mwananchi wa kawaida hawezi kumudu ambao kwa pikipiki ni Tsh 6000 kwenda hospitali ya wilaya na kurudi.

Bi Siti aliongeza kwa kusema wanaomba haki itendeke ili kupata shamba la kijiji ili litumike kujenga zahanati kwani watapunguza  changamoto wanazokutana nazo kwa kuwa mpaka sasa Mh Diwani ameshafanikiwa kupata mabati 100 na matofali 6000 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa zahanati hiyo.

Diwani wa Kata ya Tengelea  Mh Shaban Manda anasema kwamba” baada ya kuona kuna mgogoro wa zahanati ya hoyoyo iliyojengwa na taasisi ya WAMA nikalisemea kwenye kikao cha baraza la madiwani ambapo ilipelekea  kuundwaji wa kamati ili kufuatilia kuhusu zahanati hiyo lakini tuliambiwa kwamba zahanati sio ya kwetu”

Manda aliendelea kusema Katika kuhakikisha wanaitika wito wa kuwasaidia wananchi kwenye huduma ya afya halmashauri imeahidi  kutoa  matofali 6000 na bati 100 na Mh Abdallah Ulega ameahidi kutoa mifuko 100 ya saruji.

 “Eneo hili ni la kwetu na tumekubaliana na wananchi wangu kushikamana pamoja kwakua wenzetu wanatumia nguvu ya fedha katika kufinya kupata haki yetu wananchi wa hoyoyo tunaonewa kwakua zahanati ya kwanza tuliikosa na sasa hivi wanasema shamba sio letu.”

Afisa Ardhi Mteule bwana Mussa Kichumu alisema ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashari ya Mkuranga ilipokea  barua ya malalamiko tarehe 9/07/2018 kutoka kwa Mh Diwani wa kata ya Tengelea kuhusiana na uuzwaji wa ardhi ya kijiji kinyemela.

Kichumu alisisitiza kwamba kwakua sheria ya ardhi ya vijiji Na 5 ya mwaka 1999 imewapa mamlaka  serikali ya kijiji juu ya usimamizi wote wa ardhi ya kijiji ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji iliamuandikia barua Ofisa Mtendaji wa kijiji cha hoyoyo barua ya tarehe 19/07/2018 ya kutaka kuwasilisha taarifa juu ya lalamiko hilo.

Kichumu aliongeza mpaka sasa wanaendelea kusubiri taarifa hiyo ili waone namna gani Halmashauri inaweza  kuingilia kati na kutatua mgogoro huo kwa mujibu wa sheria.

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.