• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Waziri Kairuki afanya ziara ya siku mbili Wilayani Mkuranga

Posted on: January 20th, 2020

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu ( Uwekezaji ), Angellah Kairuki amewapongeza viongozi wa Halmashauri ya Wilaya Mkuranga Mkoa wa Pwani  kwa Kuwapokea na kuwalea vizuri wawekezaji  sambamba na kuwataka kutenga maeneo ya uwekezaji na kuhakikisha wanaweka miundo mbinu stahiki ili kuongeza mapato ndani ya Wilaya hiyo.

Akiwa Wilayani Mkuranga jana kwa ziara ya siku mbili ya kutembelea baadhi ya viwanda, kwa lengo la kujionea shughuli mbali mbali zinazofanywa pamoja na changamoto wanazokumbana nazo, Kairuki amevipongeza viwanda hivyo kwa kuzaliza bidhaa bora sambamba na kulipa tozo zote za Serikali na kuvitaka baadhi ya viwanda ambavyo havijajiunga na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)  Kufanya hivyo  ili wafaidike na fursa zinazopatika katika Taasisi hiyo.

Pamoja na hayo Waziri Kairuki amewaondoa shaka wawekezaji hao kwa kutoa ahadi ya kuzichukua baadhi ya changamoto  ambazo zimeonekana ni kikwazo kikubwa na kuzifikisha katika maeneo husika ili zipatiwe ufumbuzi na hatimaye viwanda hivyo viendelee kufanya kazi kama ambavyo Raisi Dr. John Pombe Magufuli anavyotaka kwa maana ya kutekeleza Sera ya Viwanda.

Amesema  pamoja na kuwasilisha hayo pia atawasiliana na Waziri wa Mambo ya Ndani  Kangi Lugola kwa ajili ya kuona ni namna gani wataboresha jeshi la zima moto ndani ya Wilaya ya Mkuranga kwani viwanda vilivyopo ni vingi lakini kuna changamoto kubwa kwa jeshi hilo kwa kukosa vifaa vya kuzimia moto, hoja ambayo iliwasilishwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mkuranga Ally Msikamo.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga amewataka wamiliki wa Viwanda kutowafungia milango Viongozi  na Taasisi wezeshi na badala yake wanatakiwa kutoa ushirikiano ili kuendeleza mahusiano mema katika shughuli za uzalishaji mali kati ya Serikali na viongozi wa Viwanda hivyo.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mkuranga Kanyala Mahinda, ambaye pia ni Afisa Mipango amesema kwa Halmashauri hiyo inategemea mapato yake kupitia vyanzo vikuu viwili ambavyo ni madini ya mchanga na tozo kutoka viwandani ambapo kwa kipindi kilichopita 2018/2019 wamefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 1.5 na kuongeza kuwa kuna changamoto ya baadhi ya viwanda kulipa  tozo katika Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam.

Viongozi wa viwanda wametakiwa kusaidia jamii inayowazunguka kwa kuchangia maendeleo mbalimbali katika sekta ya Elimu, Afya na nyinginezo kutokana na faida wanazopata katika  bidhaa wanazotengeza katika viwanda hivyo.

waziri Kairuki katika ziara yake Wilayani Mkuranga ametembelea kiwanda cha Kubangua Korosho (Sabai), Kiwanda cha Tofali (Shafa), Kiwanda cha kutengeneza Vifaa vya umeme(Everwell) , vingine ni Kiwanda maji (Ice Drop), kiwanda cha Nondo (Lodhia ), kiwanda cha WAJA Mabati pamoja kiwanda cha Kuchakata samaki (Abajuko)

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.