Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

ZAHANATI SABA ZALETA CHACHU KWENYE HUDUMA ZA AFYA MKURANGA

Posted on: May 13th, 2020

Takribani zahanati zaidi ya saba zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga  Mkoa wa Pwani zinatarajiwa kufunguliwa mapema mwaka huu, hii ni katika kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na mh Raisi Dk John Pombe Magufuli katika kuleta maboresho kwenye sekta ya afya..

Akizunguma katika Baraza la uwasilishwaji wa taarifa za kata za robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2019/2020 lililo fanyika katika ukumbi wa Flex Garden Diwani wa kata ya Tengelea na Mwenyekiti wa kamati ya uchumi na fedha  Mh  Shabani Manda amesema amefurahishwa sana na jinsi ambavyo Mkurugenzi mtendaji  wa wilaya, sambamba na wakuu wa idara na vitengo wanavyosimamia vyema miradi inayoanzishwa na wanachi wa wilaya hiyo na hatimae kuiongezea nguvu na kuweza kufikia malengo ambayo mpaka sasa wanajivunia kupata zahanati saba ambazo wanatarajia kuzifungua na kuanza kufanya kazi mapema mwaka huu….

Aidha diwani wa kata ya Mkamba Mh. Hassani Dunda aliongeza kwa kusema anaridhishwa na maendeleo  yanayoonekana katika Wilaya hiyo haswa upande wa elimu ambapo ndani ya kipindi cha miaka mitano wameweza kujenga sekondari tatu ikiwepo shule ya sekondari ya Abdalla Ulega iliyopo kata ya Tambani, shule ya sekondari mwandege iliyopo kata ya mwandege na shule ya sekondari miteza iliyopo kata ya njia nne……

Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mkuranga na Diwani wa kata ya Magawa Mh. Juma Abeid aliongeza kwa kusema hana budi kumshukuru Mh Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kwa kuwaletea  Mkurugenzi Hodari ambaye anajitoa kwa hali na mali na kutumia mda wa ziada katika kutekeleza na kusimamia majukumu yote yanayoihusu Halmashauri hiyo bila kujali mda anaotumia hata ule ambao anapaswa kupumzika

Diwani huyo wa Kata ya Magawa aliongeza kwa kusema kuwa  anamuomba Mh Raisi Dkt. John Magufuli aendelee kumuacha Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya kwani ameonesha uadilifu na utiifu kwa kuzingatia ilani ya chama cha mapinduzi katika kusimamia miradi na kutimiza wajibu wake katika kazi..

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mhandisi Mshamu Munde aliwashukuru wakuu wa idara na vitengo kwa juhudi wanazozifanya za kusimamia miradi ya maendeleo na amewataka kusimamia ubora na viwango vya hali ya juu katika miradi yote inayoanzishwa ndani ya wilaya hiyo…..

Aidha mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mkuranga Ally Msikamo akitoa neno la shukrani amesema anawashukuru  Madiwani wote, wakuu wa idara na vitengo kwa kujitoa kwa hali na mali na kuweza kusimamia ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa kipindi chote walichokua madarakani pamoja na tofauti zilizokuwepo amekiri kuwa kuna wakati tofauti za mawazo na migongano huleta umoja na mshikamano katika kutafuta maendeleo ndani ya Wilaya….

Zahanati zinazotarajiwa kufunguliwa mwaka huu ni pamoja na zahanati ya Kuruti, Nganje, Tengelea, Mwarusembe, Kimanzichana, Nyatanga na Koma…

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA 10% KWA MWAKA WA FEDHA 2024-2025

    May 20, 2025
  • RO MKURANGA AWAFUNDA WAANDIKISHAJI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI

    May 14, 2025
  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.