• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Maji

TAARIFA YA WILAYA YA MKURANGA YA HALI YA HUDUMA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI: 

 

Utangulizi:

Wilaya ya Mkuranga ina hali ya hewa ya joto la wastani wa nyuzi joto 28.Wilaya inapata misimu miwili ya mvua yaani masika na vuli.  Wastani wa mvua hizi ni milimita 800 hadi 1000 kwa mwaka.  Mvua za masika kawaida hunyesha kati ya miezi ya Machi hadi Juni, na mvua za vuli hunyesha kati ya miezi ya Oktoba hadi Desemba. Katika miaka ya hivi karibuni mvua hizo zimekuwa ni haba kutokana na mabadiliko ya tabianchi. Hali hii imechangia sana kukauka kwa vyanzo vya maji, hususan katika maeneo yenye huduma ya maji ya visima vifupi.

Vyanzo vikuu vya maji katika wilaya ya Mkuranga, ni pamoja na uvunaji wa maji ya mvua, maji ya chini ya ardhi (Underground Water), Chemichemi na Mabwawa. Mpaka Juni, 2017 jumla ya wakazi 123,623 wanapata huduma ya majisafi na salama.. Hii ni sawa na asilimia 62.5 ya wakazi wote 197,797 wa Mkuranga waishio vijijini. Vilevile asilimia kumi   (10) ya  wakazi wa Mji wa Mkuranga  ndio wanaopata huduma ya maji safi na Salama

Huduma ya Maji:

Mpaka kufikia tarehe 30 Juni 2017, huduma ya maji katika wilaya ya Mkuranga maeneo ya vijijini yamekuwa yakipata maji kwa wastani wa asilimia 62.5. Aidha, huduma hii hutolewa kwa kutumia miundombinu ya maji ya mitandao ya bomba, visima virefu na vifupi vya pampu za mkono na zinazoendeshwa na mitambo ya Genereta za nishati ya   mafuta, umeme wa nguvu ya Jua na mifumo ya kuvuna maji ya mvua. 

Aidha, jumla ya wakazi 2512 wa makao makuu ya Halmashauri ya Mkuranga, wamekuwa wakipata maji safi na salama sawa na asilimia 10 ya wakazi wote wa mji. Mji huu hupata maji kutoka katika chanzo ambacho ni kisima kirefu kilichopo eneo la Kulungu.

Jedwali namba 1 na 2 hapa chini yanaonyesha viwango vya upatikanaji wa huduma ya maji katika Vijiji na mji wa Mkuranga.

Jedwali Na 1: Viwango vya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa vijijini katika wilaya ya Mkuranga kufikia tarehe 30 Juni 2017

Na
Halmashauri
Idadi ya watu (sensa) 2012
Kiwango cha upatikanaji wa maji (%)
Waliopo
Wanaopata maji
1
Mkuranga

197,797

123,623

62.5

Jedwali Na 2: Viwango vya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa Mjini Mkuranga (makao makuu ya Halmashauri ) ya wilaya ya Mkuranga kufikia tarehe 30 Juni 2017.

 

Na
Halmashauri

Idadi ya watu (sensa) 2012

Kiwango cha upatikanaji wa maji (%)

Waliopo
Wanaopata maji
1
Mkuranga

25,124

2510

10

 

UTEKELEZAJI WA MIRADI KATIKA VIJIJI 10 KATIKA HALMASHAURI

Mkuranga ni wilaya mojawapo katika Mkoa wa Pwani inayotekeleza miradi ya maji vijijini chini ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP). Katika hatua za awali za utekelezaji wa programu hii, kumekuwa na utekelezaji wa miradi midogo inayoleta matokeo ya haraka. Miradi hii ilitekelezwa katika miaka ya 2007/2008 na 2008/2009. Fedha za kutekeleza miradi hiyo zilisitishwa kutolewa mwezi Juni 2009 ili kuanza kutekeleza miradi mikubwa ya vijiji 10 katika kila Halmashauri kupitia WSDP katika mpango  wa Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RWSSP). Vijiji vilivyopewa kipaumbele ni kama ilivyoonyeshwa kwenye Jedwali Na 3 hapo chini.

Jedwali Na. 3: Vijiji Vilivyopewa Kipaumbele na Halmashauri katika kutekeleza Programu - Awamu ya Kwanza.

HALMASHAURI

VIJIJI

Mkuranga
Kilamba, Mvuleni, Kilimahewa kusini, Mandimkongo, Mandimpera, Tundu, Tipo, Bupu, na Nyanduturu

Jedwali Na 4: Hatua ya utekelezaji wa miradi ya maji vijijini kwa mpango wa vijiji 10 katika Halmashauri kupitia WSDP hadi   30 June 2017 

Halmashauri
Jina la mradi
Vijiji husika
Asilimia ya utekelezaji
Maoni
Mkuranga
Mradi wa maji ya bomba wa Kilamba
Kilamba

100

Mradi umekamilika.
Mradi wa maji ya bomba wa Mvuleni/Kilimahewa kusini
Mvuleni na Kilimahewa kusini

100

Mradi umekamilika.
Mradi wa maji wa visima 9 vya pampu za mkono.  
Mandimkongo,Tundu Mamdimpera, na Kilimahewa kusini

100

Mradi umekamilika.
Mradi wa maji ya bomba wa Bupu.
Bupu

100

Mradi umekamilika.
Mradi wa maji ya bomba wa Nyanduturu.
Nyanduturu

100

Mradi umekamilika.
Mradi wa maji ya bomba wa Tipo.
Tipo

100

Mradi umekamilika.

Maandalizi ya utekelezaji wa programu ya maendeleo ya sekta ya maji (WSDP) awamu ya pili

Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga imeainisha vijiji 8 vitakavyotekelezwa miradi katika awamu ya pili ya  program (WSDP II).

Utekelezaji: Kufikia Juni 2018 Wilaya ya Mkuranga  inatarajia kutekeleza miradi katika jumla ya vijiji 8 ambavyo vitapatiwa Maji safi na Salama kupitia program ya maendeleo ya sekta ya maji awamu ya pili (WSDP II), Vijiji hivyo ni Mkerezange, Kimanzichana, Ng’ole, Mdimni, Mwanambaya, Yavayava, Mlamleni na Mbulani mpaka sasa tayari shughuli ya uchimbaji wa visima katika vijiji hivyo umekamilika kwa asilimia 100, kazi iliyopo mbele yetu tunatengemea kuanza kufanya Usanifu wa miradi mapema pindi tu tutakapopokea fedha kwa ajili ya Usanifu wa Miradi hiyo.

  Lengo ni kuongeza huduma ya maji kutoka asilimia  62.5 mwaka 2017 hadi asilimia 70.5 ifikapo mwezi Juni 2018 .

JEDWALI No 5 LA MIRADI MIPYA INAYOTARAJIWA KUTEKELEZWA 2017-2018

 

Jina la kijiji
Jina la mradi
Kazi iliyofanyika
Kazi inayotarajiwa kuanza
Idadi ya watu wakaopata huduma ya maji baada ya kukamilika kwa mradi
Idadi ya vituo vitavyojengwa
Kimanzichana
Kimanzichana
Uchimbaji umekamilika
Usanifu wa Mradi

15,456


Mkerezange
Mkerezange
Uchimbaji umekamilika
Usanifu wa Mradi

1,397

Ng'ore
Ng'ore
Uchimbaji umekamilika
Usanifu wa Mradi

1,021

Mdimni
Mdimni
Uchimbaji umekamilika
Usanifu wa Mradi

1,032

Mwanambaya
Mwanambaya
Uchimbaji umekamilika
Usanifu wa Mradi

4,823

Yavayava
Yavayava
Uchimbaji umekamilika
Usanifu wa Mradi

993

Mlamleni
Mlamleni
Uchimbaji umekamilika
Usanifu wa Mradi

7,886

Mbulani
Mbulani
Uchimbaji umekamilika
Usanifu wa Mradi

2,561

JUMLA

35,169

70

UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAJI KUPITIA MAPATO YA NDANI ( OWN-SOURCE) NA RUZUKU KUTOKA SERIKALI KUU (LGCDG) .

 

Katika kutekeleza Miradi ya maji vijijini  Wilaya ya Mkuranga imekuwa ikitenga fedha kupitia mapato ya ndani na fedha za ruzuku kutoka serikali kuu ili kuwezesha huduma ya upatikaji wa Maji safi na salama kwa wananchi.

Hadi kufikia Juni 2017 Jumla ya Miradi 4 imekekelezwa kupitia mipango hiyo

Jedwali No 6

Jina la kijiji
Jina la mradi
Kazi iliyofanyika
Hatua iliyofikiwa
Mkerezange
Mkerezange
Ujenzi wa Mradi mdogo wa Maji (unatumia Generator)

100

Panzuo
Panzuo sekondary
Ujenzi wa Mradi mdogo wa Maji (unatumia nguvu ya jua)

100

Mkuranga
Mradi wa Maji Sokoni
Ujenzi wa Mradi mdogo wa Maji (unatumia Generator)

100

Mkwalia Kitumbo
Kulungu
Uchimbaji wa kisima

100

Nasibugani
Nasibugani Sekondari
Ujenzi wa Mradi mdogo wa Maji (unatumia Generator)

100

UTEKELEZAJI   WA MIRADI YA MAJI KUPITIA WADAU WENGINE WA MAENDELEO .

Katika Wilaya Mkuranga wapo wadau mbalimbali walioshirikiana na serikali katika kuwapatia maji wakazi wa wilaya hii ambao ni pamoja na:

Shirika la ushirikiano wa kimataifa la Japan (JICA) ambalo limejenga miradi ya maji ya bomba katika vijiji vya Mwandege/Kipala, Vianzi, Mfurumwambao/Marogoro, Kisemvule na Njopeka inayotumia umeme wa jenereta.

Aidha shirika la AFRICAN REFLECTIONS wamejenga miradi midogo midogo ya maji ya bomba katika maeneo yafuatayo ambayo ni:

Kiparang'anda, Kisima Sekondari, Nyatanga, Dundani Shule ya Msingi, Ngunguti Shule ya Msingi, Kiguza Shule ya Msingi, Vianzi Shule ya Msingi, Misasa Shule ya Msingi, Zahanati ya Lukanga na Zahanati ya Mbezi Msufini.

 miradi hii hutunmia umeme wa nguvu za jua,

HUC ( HELPED UNDESERVED COMMUNITIES) Shirika hili limeweza kushirikiana na Halmshauri kwa kuchimba visima vifupi zaidi ya 40 katika Kata ya Mkuranga, Nyamato, Bupu, Dundani, Kisiju, Panzuo, Kimanzichana Tambani, Kitomondo, Njianne Mbezi na Shungubweni   na kufunga Pampu za mikono.

BALOZI WA KUWEIT:

Balozi wa Kuweit kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Tanzania ameweza kuchimba visima sita (6) ambavyo ni  Zahanati ya Kalole, Vijiji vya Msonga, Kisayani, Shungubweni na Kerekese Shule ya Msingi.

UUNDAJI NA USAJILI WA JUMUIYA ZA WATUMIA MAJI KATIKA WILAYA YA MKURANGA

Kuunda na kusajili vyombo vya uendeshaji (COWSOs) na usimamizi wa miradi ya maji 8 ifikapo mwezi Juni mwaka 2018.

Utekelezaji: Uundaji na usajili wa jumuia za watumiaji maji umepangwa kufanyika mwaka 2017/2018 na kuendelea. Hata hivyo, kufikia mwezi Juni 2017 jumla ya Vyombo huru 22 vya watumiaji maji viliundwa na 14 kusajiliwa.

HALI YA UPATIKANAJI WA FEDHA.

Katika kipindi cha mwaka 2016/2017 Halmashauri ilitengewa  kiasi 1,187,360,000 cha fedha kilichopelekwa kwenye Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga ni shilingi 102,230,000 Kiasi cha fedha zinazotengwa kwa ajili ya halmashauri kinazingatia kiwango kilichopo cha huduma ya maji, wingi wa watu, aina ya teknolojia inayotumika na kufuzu au kutofuzu vigezo vya kupata ruzuku ya maendeleo kutoka serikalini kwa kila Halmashauri. Fedha zilizotengwa kwa ya utekelezaji wa vijiji 8 kwa mwaka 2017/2018 ni kama inavyoonyeshwa kwenye Jedwali No 9 hapo chini.

Fedha Zilizotengwa na zilizopokelewa  kwa Mwaka 2016/2017 kwa ajili ya Utekelezaji wa Miradi Jedwali No. 8


Halmashauri
Aina
Fedha zilizotengwa 
Fedha zilizopokelewa
Asilimia

Mkuranga

DC

1,187,360,000

102,230,000

8.6


Jedwali No. 9: Fedha Zilizotengwa kwa Mwaka 2017/2018 kwa ajili ya Utekelezaji wa Miradi ya Vijiji 8

Jedwali No. 9


Halmashauri
Aina
Fedha zilizotengwa 
Fedha zilizopokelewa
Asilimia
Mkuranga

DC

803,656,000

-

0


CHANGAMOTO

Pamoja na mafanikio yote yaliyopatikana katika kutekeleza miradi, kuna changamoto zililzojitokeza kama ifuatavyo:-

Upungufu wa watumishi katika idara ya maji

Uchakavu wa miundombinu ya maji hasa mjini Mkuranga

Kutopatikana fedha kwa ajili ya mradi wa maji mjini Mkuranga ili kupanua huduma

Kuchelewa kupata fedha za kulipa wakandarasi pindi wanapomaliza kazi

Baadhi ya vyombo vya watumia maji kutomudu vema majukumu yao ya kusimamia miradi

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • SILAA AELEKEZA TCRA KUFIKA RADDY FIBER MKURANGA

    June 18, 2025
  • RC KUNENGE AIPONGEZA MKURANGA KUPATA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • UWT YAZINDUA KAMPENI YA UTOAJI ELIMU ILANI YA CCM

    June 11, 2025
  • PROFESA NAGU APONGEZA HUDUMA ZA MAABARA MKURANGA

    June 05, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.