• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

'DAY CARE CENTERS' zapewa somo juu ya malezi sahihi ya watoto na vituo

Posted on: January 13th, 2019

Ofisi ya Afya kupitia kitengo cha Ustawi wa jamii kwa kushirikiana na Mganga mkuu Halmashauri wilaya ya Mkuranga, imeendesha mafunzo elekezi kwa walezi na wamiliki wa vituo vya malezi kutwa (Day care Centres) ndani ya wilaya ya Mkuranga ili kutatua changamoto mbalimbali zinazovikabili vituo hivyo na watoto wanaolelewa katika vituo hivyo

Mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa ‘Resources Centre’ Kiguza Wilayani Mkuranga yalikua na lengo ya kutatua changamoto  mbalimbali ikiwamo majengo wanayofundishia,  walimu wanaofundisha pamoja na mbinu za kufundishia ili kupata muongozo na uelewa wa pamoja juu ya uendeshaji vituo hivyo

Akizungumza mara baada na mafunzo hayo Afisa Afya Mwandamizi, Bw. Elinas Jacob Nnko alisema, kama idara waliona iko haja ya kuendesha mafunzo hayo kwani miaka miwili iliyopita ndio kulianza kuwa na vituo hivi lakini tatizo ikawa wamiliki wengi kuwa hawajui namna sahihi  ya kuendesha vituo hivyo na walikua hawajui miongozo kuhusiana na uendeshaji wa vituo vya watoto kutwa. 

“ilikaa kamati ndogo ikishirikisha Afisa Afya, Afisa Ustawi wa jamii na wadau wengine ikajadili ikaona sasa iwakutanishe hawa wadau ili wawe na uelewa wa pamoja kuhusu vituo vya kulea watoto kutwa na maeneo ya makazi kwa watoto wanaoishi mazingira magumu ili sasa pale miongozo mbalimbali na serikali na wadau wanapotaka kutoa elimu tuwe na uelewa wa pamoja  na tuwe tunaelewa nini maana ya vituo hivi” alifafanua Bw. Nnko.

Naye, Afisa Ustawi Halmashauri (W) Mkuranga Bi. Happyness Aloyce alisema,  msukomo wa kufanya mafunzo hayo pia ulitokana na mkanganyiko uliokuwepo kwa wamiliki wa vituo kushindwa kutofautisha vituo vya malezi kutwa ‘Day Care Centres’ na shule za watoto ‘Nursery schools’, huku akipongeza muitikio mkubwa wa washiriki na kutoa wito kwa washiriki hao kwenda kuyafanya kwa vitendo yale waliyojifunza

Kwa upande wake Walter Meer, mshiriki kutoka shirika la ‘Marafiki wa Watoto’ linalojishughulisha na kusaidia watoto wenye saratani na mgongo wazi pamoja na kituo cha malezi ‘Mwanangu Day Care’, alishauri vituo vingine kuanza kujumuisha watoto wenye ulemavu na sio kuchukua watoto wasio na ulemavu pekee kwani bado kuna tatizo kubwa la watoto wenye ulemavu kufungiwa ndani

Aliongeza kuwa lengo la vituo hivyo ni kuandaa watoto kimalezi hivyo watoto wenye ulemavu wanahitaji fursa hiyo pia ambapo itawasaidia sana kujitambua na kupata ujuzi wa kimaisha ili waweze kujisaidia wenyewe kwa sasa na hata siku za usoni.  

Vilevile Bi. Eliashukuru Tito ambaye ni mdhibiti Ubora katika Halmashauri Wilaya Mkuranga, alipongeza mafunzo hayo na kusisistiza washiriki kuzingatia suala la usafi na kuandaa maeneo rafiki ya michezo katika vituo vyao.

Mafunzo hayo yalifanyika kwa siku mbili ambapo mada mbalimbali zilitolewa kwa washiriki zikilenga zaidi kuboresha malezi ya watoto katika vituo hivyo

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.