• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

“UONGOZI NI DHAMANA TUCHAPE KAZI" ULEGA

Posted on: June 10th, 2020


“Nyinyi wote ni wachunga na mtaulizwa kwa vile mlivyo vichunga”, haya ni maneno yaliyotamkwa na Mh. Abdallah ulega, Naibu waziri wa mifugo na uvuvi na Mbunge wa Jimbo Mkuranga Mkoa wa Pwani wakati akilihutubia Baraza Maalumu la Madiwani liiloketi leo katika ukumbi wa Flex Garden kwa dhumuni la kujadili masuala ya kinidhamu.

Ulega alitamka maneno hayo kwa lengo la kuwakumbusha waheshimiwa madiwani ya kuwa lengo lililowaweka katika kiti hiko kwa kipindi chote  cha miaka mitano ni kuwaongoza na kuwahudumia wananchi wa Mkuranga katika kuwaletea maendeleo na kutimiza ahadi walizoziahidi kwa wananchi kabla ya kuwa madiwani, hivyo basi amewataka wale watakaorudi tena, warudi kwa lengo la kufanya kazi kwa weledi ili kuipeleka mbele Wilaya ya Mkuranga kwa kuwa dhamana ya maendeleo ipo mikononi mwao,  “ninafahamu weledi wenu na uchapakazi wenu nendeni mkafanye kazi”alisisitiza

Aidha, Naibu waziri hakusita kumpongeza pia Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mhandisi Mshamu Munde pamoja na watendaji wake wote kwa kuonesha ushirikiano wa dhahiri na kufanikisha baadhi ya miradi mbali mbali iliyoanishwa wilayani hapo lakini amemtaka Mkurugenzi kuendelea kusimamia yale yote ambayo wanayaacha kwa kipindi chote watakachokua katika harakati za uchaguzi na kumtaka kusimamia vyema bila kujisahau kwa kuwa wao hawatakuwepo…

Mh. Ulega aliona mbali zaidi kwa kusema wananchi wa Mkuranga wanaakili zao timamu wanaelewa walikotoka waliko na wanakotaka kwenda hivyo hata wanapoenda kuwania nafasi mbali mbali wajitathimini wakijua watu wanaowaomba dhamana ya uongozi ni wenye uelewa na wenye upeo chanya wa kutaka kuona maendeleo yanafanyika na sio maneno mengi kama ilivyozoeleka, alisisitiza “tuchape kazi hiyo ndo njia pekee itakayofanya tuendelee kuaminika na wananchi waliotupa dhamana ya kuwaongoza’….

Sambamba na hilo Mhandisi Munde alilihakikishia baraza hilo tukufu la madiwani akisema “tutasimamia yale yote ambayo yanatakiwa kuendelea kufanyika kwa kipindi chote ambacho hamtakua pamoja nasi na yale yote mliyoyazungumza tunayaunga mkono na tutayaendeleza kwa uadilifu”.

Baraza la madiwani linatarajiwa kufikia ukomo mapema mwezi huu kwa kuzingatia tamko la Waziri  wa TAMISEMI Mh. Selemani Jaffo…

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.