• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • TASKSMIS |
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Rasimali watu na Utawala
      • Industrial, Trade and Investment
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Mipango,Sera na Takwimu
      • Ardhi na Maliasilli
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Uongozi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Sera
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Photo Galley
    • Habari Mpya
    • Matukio

Wakulima watakiwa kuchukulia uwepo wa wafugaji kama fursa

Posted on: January 24th, 2019

Wakulima wa Vijiji vya Bupu, Panzuo na Chamgoi Wilayani Mkuranga wameshauriwa kutumia uwepo wa wafugaji katika vijijini vyao kama fursa ya maendeleo na sio kuwaona kama maadui hali inayopelekea kuwa na migogoro ya mara kwa mara

Akiongea katika mikutano ya hadhara iliyofanyika katika vijijini hivyo, Katibu Mkuu chama cha wafugaji Tanzania Ndg. Magembe Makoye ambaye pia ni mjumbe kamati ya usuluhishi migogoro kati ya wakulima na wafugaji nchini Tanzania, alisema, wakulima ndani ya vijiji hivyo hawana budi kuanza kuchukulia uwepo wa wafugaji katika maeneo hayo kama fursa ambayo itawapatia kipato kwa kufanya shughuli / biashara zinazohusisha mifugo hiyo 

“Vijana wa Chamgoi tuanze kujiuliza kwanini wenzetu wafugaji wana pesa mwaka mzima? Basi tuiangalie hiyo kama fursa, mifugo ni pesa! Kama una eneo la ekari kadhaa unaweza kulizungushia na kukodisha kama eneo la malisho kwa wafugaji, hiyo ni pesa tayari” alisisitiza bwana Makoye

Aliongeza kwa kuwashauri wafugaji  kufuata taratibu sahihi za kuingia katika vijiji hivyo  ili waishi kwa mfumo sahihi tofauti na sasa wanavyojitenga hali inayohatarisha maisha yao, akitolea mfano wajawazito wa jamii hizo kujifungua katika mazingira magumu kwani wako mbali mno na vituo vya afya.

Jitihada hizi za kutatua migogoro hii zimekuja baada ya kuibuka mapigano kati ya wakulima na wafugaji mwishoni mwa mwaka jana ambapo kuliibuka mapigano kati ya wakulima na wafugaji jamii ya wamang’ati na ndipo Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Mbunge wa Mkuranga Mh Abdallah Hamis Ulega kumuagiza katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuunda timu ya wataalam ambao watashughulikia mgogoro kati ya wakulima na wafugaji katika Mkoa wa Pwani.

Kamati hiyo inayohusisha wajumbe kutoka wizara mbalimbali ikiwamo Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya makazi, Wizara ya Mambo ya ndani , Wizara ya Kilimo na Mifugo pamoja na Ofisi ya Rais inashirikiana na idara ya Kilimo na Mifugo pamoja na Idara ya Maliasili (Misitu) Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga  kufanya ziara maeneo yenye migogoro kati ya wafugaji na wakulima ili kupata suluhu ya pamoja

Matangazo

  • TANGAZO LA VITUO VYA USAILI January 21, 2025
  • ORODHA YA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA January 21, 2025
  • Tazama vyote

Habari Mpya

  • MADIWANI MKURANGA WAPITISHA TAARIFA YA MAENDELEO ROBO YA TATU

    April 29, 2025
  • KIJANA WA MLENGWA WA TASAF ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

    March 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA IMEFANYA UZINDUZI WA MIRADI YA (TI)

    March 01, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA

    February 10, 2025
  • Tazama vyote

Video

SIMAMIENI MAADILI
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya Ruhusa ya Ugonjwa kwa Watumishi (Sick Sheet Form)
  • FFARS user manual
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2020/2021 Mkuranga
  • Barua pepe za ofisi za watumishi
  • Fomu ya Likizo kwa Watumishi
  • Fomu ya Ruhusa kwa Watumishi
  • Fomu ya Maombi ya Leseni ya Biashara

Tovuti Linganifu

  • TAMISEMI
  • e-GA
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ajira
  • Ikulu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Baraza la Mitihani la Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
  • Mkuranga Tasks Management Information System (Tasks MIS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga

    Postal Address: P. O. Box 10, Mkuranga, Pwani, Tanzania

    Telephone: +255232110038

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@mkurangadc.go.tz; ded.mkuranga@pwani.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Copyright ©2023 MkurangaDc. All rights reserved.